Mary Mtuka
MKAZI wa Kinondoni 'B' Jijini Dar es
Salaam Sajala Binde (34), amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu
Mkazi Kinondoni akituhumiwa kumwingilia kinyume na maumbile mwanamke mmoja
(jina limehifadhiwa).
Akisoma hati ya mashtaka mbele ya Hakimu
wa Mahakama hiyo Is -Haq Kuppa, Wakili wa Serikali, Joseph Nasuwa alidai kuwa
tukio hilo lilitokea Juni 6 mwaka huu maeneo ya Kinondoni Biafra.
Baada ya kusomewa hati hiyo ya mashitaka,
mtuhumiwa alikana kutenda kosa hilo na Wakili alidai upelelezi bado unaendelea.
Hakimu Kuppa alisema shtaka hilo
linadhaminika kisheria, hivyo alimtaka mtuhumiwa kuwa na wadhamini wawili wenye
barua ya utambulisho na kujidhamini kwa Sh. milioni tano kila mmoja.
Hata hivyo, mshitakiwa huyo alishindwa masharti
ya dhamana na kurudishwa rumande ambapo Hakimu Kuppa alihairisha kesi hiyo hadi
Desemba 20, mwaka huu.
Wakati huohuo, Husaein Yusuph (17) na
rafiki yake Emmanuel Cosmas wamepanaishwa kizimbani katika mahakama hiyo
wakikabiliwa na kupatikana na madawa ya kulevya yenye uzito wa Gramu 32.1.
Wakisomewa maelezo ya kosa mbele ya
Hakimu Boniface Lihamwike, Wakili wa Serikali Ramadhan Mkimbu, alidai kwamba
watuhumiwa walitenda kosa hilo Novemba 13 mwaka.
Wakili Mkimbu alidai kuwa watuhumiwa
walipatikana na madawa hayo aina ya Cannabis Sativa yajulikanayo kwa jina la
Bhangi.
Baada ya kusomewa shtaka hilo kila mmoja
kwa wakati wake alikana kutenda kosa hilo na Wakili alidai upelelezi bado
unaendelea.
Hakimu Lihamwike alisema kesi hiyo inadhaminika
kisheria hivyo aliwataka watuhumiwa kuwa na wadhamini wawili wenye barua
watakao weka saini ya Sh. milioni 1 kwa kila mmoja.
Hata hivyo, kesi hiyo imeahirishwa hadi
Desemba 12 mwaka huu na watuhumiwa walirejeshwa mahabusu.







0 comments:
Post a Comment