Upelelezi kesi dhidi ya vigogo TPA bado


Grace Gurisha

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imedai mahakamani kuwa upelelezi wa kesi ya kuomba rushwa ya dola za Marekani milioni nne (zaidi ya Sh bilioni nane) inayomkabili aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA), Ephraim Mgawe, na wenzake haujakamilika.

Hayo yalidaiwa jana na Wakili wa Takukuru, Emmanuel Jacob mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba kesi hiyo ilipotajwa na kuangalia kama upelelezi umekamilika.

Baada ya Jacob kudai kuwa upelelezi haujakamilika, Hakimu alikubaliana na maelezo yao na kuahirisha kesi hiyo hadi Desemba 18 itakapotajwa tena. Mgawe anadaiwa kufanya kitendo hicho ili atoe zabuni ya ujenzi wa bomba la kupakulia mafuta.

Mbali na Mgawe, vigogo wengine ni Mkurugenzi wa zamani wa Uhandisi, Bakari Kilo (59), aliyekuwa Meneja wa Mazingira , Theophil Kimaro (54) na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya DB Shapriya, Kishor Shapriya (60).

Jacob alidai kuwa tuhuma za kuomba rushwa zinawakabili Mgawe, Kilo na Kimaro, ambao wanadaiwa kutenda kosa hilo katika tarehe tofauti na maeneo tofauti ambayo hayafahamiki kati ya mwaka 2009 na 2012.

Ilidaiwa kuwa kwa kutumia nafasi zao, waliomba rushwa ya dola hizo kupitia kwa wakala wa kampuni ya DB Shapriya kuiwezesha  kampuni  ya  DB Shapriya kupata zabuni ya ujenzi wa bomba la kupakulia mafuta kwenye rasi ya Mji Mwema kinyume na sheria ya Takukuru.

Alidai walifanya hivyo ili Shapriya ashinde zabuni iliyokuwa ikishindaniwa namba AE/0116/2008-2009/10/59.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo