Mwanasheria mkuu akana kuzuia mikopo


Peter Akaro

George Masaju
OFISI ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imesema haina mamlaka ya kuzuia wala kuruhusu mtumishi yeyote wa Serikali kukopa au kutokukopa katika taasisi yoyote ya kifedha nchini.

Imetoa kauli hiyo baada ya siku za karibuni kuenea taarifa iliyodaiwa kutoka ofisi hiyo kuwa Serikali imepiga marufuku watumishi wa umma kukopa benki, Saccos, vicoba na taasisi mbalimbali za kifedha.

Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari ilitolewa jana Dar es Salaam na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Asiatu Msuya, taarifa hiyo siyo ya kweli.

“Ikumbukwe kuwa mikopo yote ya watumishi wa umma katika taasisi za fedha hutolewa kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizopo ili mradi mtumishi awe ametimiza vigezo,” alisema.

Msuya aliongeza kuwa watumishi wa umma wasijihusihe na usambazaji wa taarifa zisizo za kweli na ambazo hazijatolewa na mamlaka husika.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo