JPM ateua makatibu tawala kujaza wilaya 27


Mwandishi Wetu
Dk. John Magufuli

OFISI ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imetangaza uteuzi wa makatibu tawala wa wilaya 27 kujaza nafasi zilizokuwa zimeachwa wazi.

Makatibu tawala hao na wilaya zao katika mabano ni Timotheo Mzava (Arumeru, Arusha), Fabian Sospeter (Nyangw’hale, Geita ), Innocent Nsena (Karagwe), Abdallah Mayomb (Misenyi), Greyson Mwengu (Kyerwa), Agnes Mwakyoza (Biharamulo), Mbwana Kambangwa (Liwale), Agenellus Mwakitalu (Kilwa), Sarah Sanga (Hanang’), Paul Bura (Mbulu), Yohana Kastila (Kilosa).

Wengine ni Robert Selasela (Kilombero), Lameck Lusesa (Malinyi), Palango Abdul (Nanyumbu), Bosco Bugali (Misungwi), Menruf Nyoni (Magu), Said Kitinga (Ilemela), Grace Mgeni (Makete), Zaina Mlawa (Ludewa), Milongo Sanga (Kibiti), Frank Sichalwe (Kalambo), Nicodemas Mwikozi (Meatu), Filbert Kanyilizu (Itilima).

Pia wamo Godwin Chacha (Busega), Winfrida Funto (Ikungi), Elizabeth Rwesagira (Mkalama), Michael Nyahenga (Kaliua).

Taarifa iliyotolewa jana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angela Kairuki inawataka makatibu tawala hao kufika kwa Katibu Mkuu wa Wizara wakiwa na wasifu wao (CV) na nakala za vyeti vyao vya kielimu.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo