Serikali yapiga marufuku uuzaji vilainishi


Abraham Ntambara

Dk Hamisi Kigwangala
SERIKALI imepiga marufuku uuzaji wa vilainishi vya kupima unaofanyika mtaani na sokoni kwa sababu vifungashio vya vilainishi hivyo havikidhi ubora na vinaharibu vilainishi ambavyo huathiri utendaji wa mitambo.  

Aidha, imemwagiza Mkemia Mkuu wa Serikali kuendelea na uchunguzi wa kimaabara wa vilainishi vilivyo sokoni, kwa kushirikiana na kampuni zenye nembo halisi ili kubaini na kutambua bidhaa za vilainishi halisi na visivyokidhi viwango vya ubora.

Kauli hiyo ilitolewa juzi Dar es Salaam kwa vyombo vya habari na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Hamisi Kigwangala, wakati akitoa tamko kuhusu ubora wa bidhaa za vilainishi nchini kwa mwaka 2013 hadi mwaka huu.

“Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kupitia Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali inatekeleza jukumu la kusimamia Sheria Namba 3 ya mwaka 2003 inayohusu Usimamizi na Udhibiti wa Kemikali za Viwandani na Majumbani.

“Lengo kuu la kuanzishwa kwa sheria hiyo ni kuhakikisha nchi inalindwa ili isiwe soko la bidhaa hafifu,  kemikali zinazoingia na kutumika nchini ziwe zenye ubora na salama katika kulinda afya na mazingira,” alisema Dk Kigwangala.

Alisema Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali ilipofanya ufutiliaji wa ubora wa vilainishi vinavyouzwa sokoni na kuvifanyia uchunguzi ili kubaini kama vimekidhi viwango vya ubora katika Jiji la Dar es Salaam, na kufanyiwa uchunguzi wa kimaabara, ilibaini asilimia 50 ya vilainishi vya injini na petroli zilizochunguzwa ilionekana kutokidhi viwango vya ubora.

Aidha aliongeza kwamba asilimia 52.6 ya vilainishi vya injini, aina ya dizeli vilivyochunguzwa vilionekana kutokidhi viwango vya ubora vya vilainishi vya kitaifa huku asilimia 77.7 ya vilainishi aina ya ATF vilionekana kutokidhi viwango vya ubora.  
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo