Utafiti wabaini viashiria hatarishi vya magonjwa


Leonce Zimbandu

Dk Tatizo Waane
MWENYEKITI wa Shirikisho la Vyama vya Magonjwa yasiyo ya Kuambukiza (TANCDA), Dk Tatizo Waane, amesema utafiti uliofanywa kwenye wilaya 53 nchini, umeonesha viashiria hatarishi vya magonjwa yasiyo ya kuambukiza, ikiwamo kisukari, saratani na ugonjwa wa moyo.

Utafiti ulifanyika 2012 na kuonesha viashiria vya magonjwa hayo, huku asilimia ikiwa kwenye mabano, unene kupita kiasi (26), shinikizo la damu (26), mafuta mengi mwilini (33.8) na kisukari (9.1).

Pia utafiti huo ulibaini wananchi wanaovuta sigara (asilimia 25.9), pombe (asilimia 29.3) na wanaokula mboga mboga na matunda chini ya mara tano kwa siku ni asilimia 97.2.

Waane alisema hayo alipozungumza na gazeti hili Dar es Salaam mwishoni mwa wiki kwenye uzinduzi wa kampeni ya mazoezi na kutoa fursa kwa wananchi kupima afya zao bure.

Alisema katika utoaji huduma ya kupima afya bure bado kuna changamoto ya uhaba wa dawa kwa baadhi ya huduma, hivyo Serikali iliombwa kuendelea kushirikiana na wataalamu na kupokea ushauri wao.

“TANCDA tunaendelea kushirikiana na Wizara ya Afya kuongeza uelewa kwa wananchi kwa kutumia vyombo vya habari, matembezi na makongamano ili kupunguza magonjwa hayo nchini,” alisema.

Alisema magonjwa ya figo na moyo huigharimu Serikali kutibu wananchi wake nje ya nchi, hivyo kinga ni bora kuliko tiba.

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu alisema mkakati mkuu wa kufanya wananchi kufanya mazoezi utasaidia nchi kuokoa fedha na maisha ya watu wake.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo