Zitto akiri ACT kudaiwa milioni 300/-


Mwandishi Wetu

Zitto Kabwe
KIONGOZI wa ACT-WAzalendo, Zitto Kabwe, ameishauri Seikali kuandaa kanuni za kuhakikisha kila hospitali ina akiba ya kutosha ya damu ili kusaidia wagonjwa wenye kuhitaji kabla watu wengine hawajajitolea ili kuokoa maisha.

Zitto ametoa ushauri huo jana kupitia waraka wake kwa njia ya mtandao ambapo pia aliihimiza jamii kuongeza bidii ya kuchangia dau kwa hiyari kufuatia tukio aliloshuhudia katika moja ya hospitali Dar es Salaam, usiku wa kuamkia jana ambapo wazazi wawili walikuwa wakihaha kusaka msaada wa damu kuokoa maisha ya mtoto wao.

“Naishauri Serikali itengeneze kanuni za kuhakikisha kila hospitali inakuwa na akiba ya damu ya kutosha na mgonjwa mwenye kuhitaji apewe kwanza damu kabla ya kutafuta watu wa kuchangia kiwango husika.

Juhudi za kuchangia damu kwa hiari ziongezeke kama tufanyavyo wanachama wa ACT Wazalendo ambao kila mwaka wiki ya kwanza ya Mwezi Mei hujitolea damu kwa hiari kwenye hospitali za umma nchini kote,” alisema.

Zitto pia amewashauri Watanzania kujua makundi ya damu waliyonayo na kuweka kumbukumbu ili waweze kuokoa maisha yaw engine au yao pindi damu itakapotakiwa kwa haraka.

“Sasa najua Group langu, ilikuwa ni makosa makubwa na uzembe wa hali ya juu kwangu kutojua ' blood group ' yangu. Msiojua ‘blood group’, mjue sasa kwani hatujui siku wala saa,” alisema Zitto baada ya kupima na kujitolea damu kuokoa maisha ya mtoto huyo aliyejulikana kwa jina la Rahma. 

Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo