Watanzania wahadharishwa uwepo mchele wa plastiki

Jemah Makamba

Mchele wa plastiki
WATANZANIA wametakiwa kutoa taarifa wanabaini uwepo wa mchele usioeleweka, baada ya kuibuka kwa taarifa ya mchele bandia wa plastiki kukamatwa Nigeria.

Msemaji wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Gaudencia Simwanza alisema hayo jana alipozungumza na mwandishi wa gazeti hili.

Alisema wao sasa wana mifumo mizuri ya kudhibiti uingizwaji wa bidhaa zisizofaa na mpaka sasa mfumo huo haujabaini mchele wa aina hiyo nchini.

"Tunadhibiti na tuko makini kufuatilia wafanyabiashara wanaoingiza vitu haramu na kama huo mchele ungekuwa umeingia, tungeshajua," alisema.

Mwandishi wa habari hii alipomwuliza ikitokea umeingizwa kimagendo nchini, Watamzania watautambua vipi, Gaudencia aliwataka kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa watakapoona mchele wasiouelewa.

Mchele huo bandia ulikamatwa na Mamlaka ya Mji wa Lagos, Nigeria wiki hii, ambapo walikamata magunia 102.

Taarifa kutoka nchini humo, zilieleza kuwa uliingizwa nchini humo na wafanyabiashara haramu na unafanana na mchele wa kawaida, hivyo ni ngumu kuutofautisha na mchele wa kawaida.

Kutokana na kusambaa kwa kasi kwa mchele huo, huwezi kuutambua kwa haraka hadi pale unapopikwa ndipo unaweza kuona ni mchele wa plastiki. Hata hivyo baadhi ya wataalamu walisema kabla ya kuupika mchele huo ukilowekwa kwenye chombo chenye maji unaelea tofauti na halisi ambao huzama.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo