Mwinyi aongoza mamia kumzika Mtulia


Hajji Kameta, Daystar

Ali Hassan Mwinyi
RAIS mstaafu Ali Hassan Mwinyi ameongoza mamia ya wakazi wa Dar es Salaam na Pwani kwenye maziko ya aliyekuwa daktari wake, Profesa Idrisa Mtulia ambaye alifariki dunia nyumbani kwake juzi.

Pamoja na Mwinyi, walikuwapo pia Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, Kingunge Ngombale-Mwiru, Adam Malima na Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete.

Wengine ni Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa, Waziri wa Ulinzi, Dk Hussein Mwinyi, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani,  Hamad Yussuf Masauni na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Mpoki Ulisubisya.

Akizungumza kwenye maziko hayo Shekhe wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum alisema Mtulia alikuwa kiongozi mcha Mungu hivyo ni vema kila mwanadamu akaishi kwenye misingi hiyo.

Shekhe Mussa alisema ni vema kila mtu akajiandaa kwa kifo, kwani kinakuja bila taarifa hivyo ni vema kufanya ibada ili kuvuna mema ahera.

Kinana amemtumia salamu za rambirambi Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Pwani, Mwishehe Mlao akisema marehemu alikuwa mmoja wa wanachama waliotumikia chama na Serikali kwa uadilifu wa hali ya juu, akiwa pia Mwenyekiti wa Bohari Kuu ya Dawa (MSD).

Profesa Mtulia alipata kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM kuanzia mwaka 2002 hadi 2007. Ameacha mjane na watoto sita.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo