Majina ya biashara, kampuni 500 yasajiliwa


Mwandishi Wetu, Rukwa

Loy Mhando
MAJINA ya biashara na kampuni 495 yamesajiliwa katika kipindi cha siku 90 za  kampeni  ya  mkoa kwa mkoa inayofanywa na  Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela), ili kuhamasisha wafanyabiashara.

Kaimu Meneja Miliki Ubunifu wa Brela, Loy Mhando, alibainisha hayo jana kwamba kati ya idadi iliyosajiliwa, 72 ni kampuni na 423 ni majina ya biashara na kampeni hiyo imepata mafanikio.

 “Tunaendelea vizuri, mwamko wa wafanyabiashara ni mkubwa kwani wanajitokeza,” alisema Loy akifafanua kwamba katika kampeni hiyo wafanyabiashara hupewa elimu kuhusu umuhimu wa kusajili biashara zao.

Alisema kampeni hiyo imefanyika Geita, Simiyu, Mwanza, Mara, Mbeya, Songwe na Rukwa ambako wafanyabiashara wamekuwa wakitoa ushirikiano mkubwa kwa maofisa wa Brela.

Akizungumzia usajili wa majina ya biashara, Loy alisema kampeni hiyo ni endelevu kwa nchi nzima na itaambatana na utoaji elimu kwa wafanyabiashara juu ya muhimu wa kurasimisha biashara zao na kutambuliwa na mamlaka husika.
  
Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa, Tixon Nzandy alisema ujio wa maofisa wa Brela mkoani mwake ni fursa ya kuleta mabadiliko ya kiuchumi.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo