Abraham Ntambara
Angella Kairuki |
WAZIRI wa Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angella Kairuki, amemwagiza Mkurugenzi
Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kuwasimamisha kazi maofisa
washauri na ufuatiliaji 106 kwenye halmashauri walioshindwa kufuatilia na
kusimamia Mpango huo.
Aidha,
amemtaka kuwasimamisha maofisa watano wa makao makuu wanaosimamia mpango huo
pamoja na Meneja wa Uratibu na Mkurugenzi wa Uratibu ambao ndio viongozi
wasimamizi wao wakuu.
Waziri
Kairuki alitoa kauli hiyo jana Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na vyombo
vya habari akimtaka Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF kuhakikisha uchunguzi
unakamilika katika kipindi kisichozidi mwezi mmoja kuanzia jana.
“Naagiza
ufanyike uchunguzi wa kina ili kubaini ushiriki wa maofisa hao na kuchukua
hatua stahiki kwa watakaothibitika kuhusika na usimamizi, ufuatiliaji na
uwajibikaji,” alisema Kairuki.
Aliongeza
kuwa kwa kushirikiana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- TAMISEMI tayari
ameelekeza waratibu wa TASAF wa Wilaya wasimamishwe kazi na uchunguzi wa jinsi
walivyojihusisha kuvuruga utekelezaji wa Mpango huu, hadi kuandikisha kaya
zisizo na sifa.
Aliitaka
TASAF makao makuu waendelee kushirikiana na halmashauri kuongeza udhibiti wa
fedha wa malipo na kuhakikisha fedha zinalipwa kwa kaya zenye sifa, ambapo
anayelipwa atalazimika kuwasilisha vitambulisho visivyopungua viwili.
Waziri
Kairuki alifafanua kuwa vitambulisho hivyo ni pamoja na cha Mpango na
kitambulisho kingine kinachotambulika na Serikali kama cha mpiga kura na cha Taifa
ili kuwa na uhakika kuwa fedha zinalipwa kwa mhusika sahihi.
Aliielekeza
TASAF makao makuu kuendelea kushirikiana na halmashauri zote kukamilisha
uhakiki wa nyumba kwa nyumba katika halmashauri nchini kabla ya malipo
yanayofuata kati ya Januari na Februari.
Aidha,
alisisitiza kuwa wakuu wa mikoa, wilaya na wakurugenzi wa halmashauri, majiji,
manispaa, miji na wilaya wahakikishe fedha zilizotolewa kwa kaya zisizo na sifa
zinarejeshwa ili zinufaishe wengine.
Pia
alitoa rai kwa watumishi wa TASAF na wa halmashauri wanaohusika na mpango wa
TASAF kuwa waaminifu, waadilifu na kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za
utumishi wa umma pamoja na zile zinazosimamia mpango huo na kwamba Serikali
haitawavumilia wa kusita kuchukua hatua dhidi ya yeyote atakayekiuka Taratibu
zilizowekwa za Mpango huo.
Aidha,
alisema baada ya uhakiki kufanyika kaya 55,692 zeliondolewa kwenye Mpango
kutokana na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kaya kuhama kijiji/mtaa,
kutojitokeza mara tatu mfululizo kupokea msaada, vifo na kaya zingine kukosa
sifa.
0 comments:
Post a Comment