Kamati yasema nchi inapoteza mapato mengi ya mafuta



KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imesema Tanzania inapoteza kiasi ki­kubwa cha mapato kutokana na kushindwa kuhifadhi mafuta yanayoingizwa nchini hivyo kusababisha waagizaji kuhifadhi kwenye maghala binafsi. 

Kauli hiyo ilitolewa juzi na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Dotto Biteko alipokuwa aki­fanya majumuisho ya vikao vya kamati hiyo kwa waandi­shi wa habari.

“Kamati inaisisitiza Serikali kujenga mahali maalumu pa kuhifadhi mafuta yanayopa­kuliwa kutoka kwenye meli, kabla ya kwenda kwa wanunu­zi ili kuisaidia kuwa na uhaki­ka wa kiasi cha mafuta yaliyo­agizwa nchini,” alisema.

Aliongeza kwamba hilo pia litasaidia kupata uhakika wa kodi stahiki za Serikali kujua kama zimelipwa, usalama pamoja na kuondoa mianya ya wizi inayoweza kujitokeza.

Biteko ambaye pia ni Mbunge wa Bukombe (CCM) alisema mafuta yanapoagi­zwa yanaposhuka bandarini yanapaswa kufika katika kituo kimoja ambacho, wafanyabi­ashara wote wa nishati hiyo watachukua.

Alisema hatua hiyo imeku­wa ikisababisha mianya ya wizi huku akiitaka Serikali ku­hakikisha inakuwa na sehemu moja ya kuhifadhia mafuta kabla hayajasambazwa.

“Kamati yetu imeafanya kazi na wadau mbalimbali wak­iwemo Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), tulipowauliza kuhusu utaratibu wa usamba­zaji mafuta, wamekiri ni Tan­zania pekee ambayo unaweza kuyaingiza nchini na kila mfanyabiashara akaweka kwe­nye ghala lake, nchi nyingine yanawekwa kwenye ghala la pamoja la Serikali kwanza kabla ya kwenda kwa wafan­yabiashara binafsi,” alisema.

Alifafanua kuwa, “kwenye mnyororo wa mafuta, TPA ndiye anahifadhi mafuta, lakini anahifadhi mafuta kidogo sana na kila muagi­zaji anahifadhi kwenye ghala lake, wakati umefika Serikali itengeneze eneo malumu la kuyahifadhi yakitoka kwenye meli”.

Alisema hali hiyo itasaidia Serikali kuwa na uhakika wa kiasi mafuta yaliyoagizwa nchini, itakuwa na uhakika wa kulipwa na kodi stahiki za Serikali, usalama wa mafuta na kuondoa mianya ya wizi mdogo mdogo unaofanyika.

Pia kamati hiyo imeiagiza Serikali kupeleka majibu ya kutosha kwa kamati hiyo kuhusu sakata zima la uagizaji mafuta mabovu na upungufu wa mafuta ya taa ili jambo hilo lisijitokeze tena nchini.

Alisema wameiomba Waka­la wa Uagizaji Mafuta wa Pamoja (PPA ) watoe maelezo ya kutosha kwa nini kulitokea changamoto ya upungufu wa mafuta ya taa nchini na hatua zilizochukuliwa.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo