Shahidi: Wadhifa ulizuia kumkamata Lissu



 Grace Gurisha

Tundu Lissu
KESI ya uchochezi inayomkabili Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema), imeanza kusikilizwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kwa polisi kukiri kutomkamata kiongozi huyo kutokana na wadhifa alionao.

Askari namba E 4128 Ndege alikiri jana mbele ya Hakimu Mkazi, Godfrey Mwambapa wakati akitoa ushahidi dhidi ya Lissu, kuwa Juni 28 kwenye viwanja vya Mahakama hiyo alishindwa kumkamata akitoa maneno ya uchochezi, kwa sababu ni kiongozi, kwa hiyo walitumia busara.

Alidai maneno hayo ni: “Mamlaka ya Serikali mbovu ya kidikteta uchwara, inapaswa kupingwa kwa nguvu zote na kila Mtanzania na kwamba kama nchi itaachwa katika utawala wa kidikteta, itaingia katika giza nene.”

"Kisheria Mrakibu Msaidizi wa Polisi Kimweri naye alikuwa na mamlaka ya kumkamata Lissu kutokana na maneno yake ya uchochezi, lakini kutokana na wadhifa alionao kwa kuwa kiongozi,   tulitumia busara ili apatikane sehemu nyingine," alidai Ndege.

Alidai kuwa baada ya kutoa taarifa hiyo kwa viongozi, walichukua hatua ya kumkamata nje ya eneo ambalo alitolea maneno hayo ya uchochezi.

Pia alidai kuwa si lazima mtu anapofanya kosa akamatwe papo hapo, kwa sababu inategemea na kosa lenyewe, kwa mfano mtu anaweza kutukana akaachwa kwa sababu ndani ya tusi husika  hakuna uzito.

Akijibu maswali ya upande wa utetezi, Ndege alidai tangu Lissu atamke maneno hayo, hajawahi kusikia yamesababisha  uvunjifu wa amani na pia hajawahi kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusu maneno hayo.

Katika kesi hiyo, inadaiwa kwa nia ya kushawishi na kufanya uchonganishi kati ya wananchi wa Tanzania na Serikali, Lissu alitoa maneno ya uchochezi.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo