Vifaa vya kuhakiki vyeti vyaibwa


Stephen Kidoyayi, Shinyanga

BAADHI ya watumishi na walinzi wa Halmashauri ya Kishapu mkoani hapa, wanahojiwa na Polisi baada ya kuibwa vifaa vinavyotumika kuhakiki vyeti kwa watumishi wa umma na kuandikisha vitambulisho vya Taifa katika Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Muliro Jumanne jana alikiri kutokea kwa tukio hilo na kueleza kwamba uchunguzi wa tukio hilo la wizi unaendelea.

Kwa mujibu wa Kamanda, vifaa viliyoibwa ni pamoja na kamera mbili na viegesho vyake na vifaa hivyo vilipotea jana asubuhi wakati wakijiandaa kuendelea na uhakiki wa vyeti na kuandikisha vitambulisho vya Taifa.

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Nyabaganga Talaba alisema vifaa vilivyoibwa ni mali ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa. (NIDA).

“Leo asubuhi Ofisa wa NIDA, alibaini kamera mbili na viegesha vyake havionekani, tunaendelea kufanya uchunguzi kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi ili kubaini wahusika na kupata vifaa hivyo,” alisema Talaba.

Hata hivyo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Stephen Magoiga alisema vifaa hivyo vilikuwa vimehifadhiwa kwenye ofisi ya Halmashauri kwa ajili ya kupigia picha za NIDA.

Baadhi ya wananchi walilielezea tukio hilo kuwa ni hujuma inayofanywa na watumishi wasiojiamini kutokana na uchakachuaji wa vyeti na vielelezo vingine vinavyowahusu ili kukwepa mkono wa sheria.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo