Mabalozi EU wavutiwa kuwekeza Tanga


Mariam Cyprian, Tanga

Balozi wa EU, Roealand Van der Greer
MABALOZI wa Jumuia ya Ulaya (EU) wamevutiwa kuwekeza viwanda mkoani hapa na kuboresha bandari ya Tanga ili kukuza uchumi wake.

Akizungumza jana, Balozi wa EU, Roealand Van der Greer alieleza azma hiyo alipoongoza ujumbe wa mabalozi wa nchi hizo kufanya ziara ya siku moja ya kukagua bandari hiyo.

"Tumewasili hapa kuangalia uwezekano wa kukuza sekta ya viwanda, tunaamini ukiwapo uwekezaji mkubwa wa viwanda, uchumi wa nchi utakua lakini pia kuna umuhimu wa kuboresha bandari ya Tanga na sisi tuko tayari kushirikiana nanyi ili kukamilisha azma hii," alisema Rowland.

Mkuu wa Mkoa Tanga, Martine Shigela alisema Serikali imejipanga kukaribisha uwekezaji mkubwa ili kuhakikisha mkoa unapiga hatua kimaendeleo, ikiwamo kuimarisha ulinzi na usalama ili mkoa uendelee kuwa na amani.

"Tuko tayari kupokea wawekezaji na maeneo yapo ya kutosha, kwani mkoa wetu ni sehemu nzuri ya uwekezaji kutokana na hali ya amani na utulivu iliyopo, Serikali inajitahidi kuimarisha ulinzi na usalama, ili kuwahakikishia usalama wananchi na wawekezaji," alisema Shigela.

Shigela aliwaeleza mabalozi hao kuhusu mradi mkubwa wa bomba la mafuta ghafi kutoka Uganda unaotarajiwa kuanza mwakani, huku pia kukiwa na uwekezaji wa viwanda vikubwa vikiwamo vya saruji.

Mabalozi hao walitembelea pia ghala la kupokea mafuta la GBP na sehemu litakakoishia bomba la mafuta.

Akisoma taarifa kwa mabalozi hao, Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Andrew Arika alisema changamoto inayoikabili ni kina kifupi jambo linalosababisha meli kubwa kutia nanga mbali.

Hata hivyo, alisema ipo mikakati ya kujenga bandari mpya ya Ndumi ambayo ina kina kirefu.

Mabalozi waliokuwa kwenye ujumbe huo ni kutoka Ufaransa, Italia, Uingereza, Hispania, Ujerumani na Finland wakati Ireland na Sweden zikituma wawakilishi.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo