Chadema yateua wabunge wa Kamati Kuu


Suleiman Msuya

Tumaini Makene
WABUNGE wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wamechagua wenzao watano watakaowakilisha kundi la wabunge kwenye Kamati Kuu ya Chama hicho.

Taarifa iliyotolewa jana na Msemaji wa Chama hicho, Tumaini Makene ilisema wabunge hao wamechaguliwa kwa mujibu wa Ibara ya 7.7.14 (g) ya Katiba ya Chadema inayotoa nafasi tano za kuchagua wajumbe wa Kamati Kuu kuwakilisha kundi hilo.

Alitaja wabunge waliochaguliwa kuwa ni Tundu Lissu (Singida Mashariki), Godbless Lema (Arusha Mjini), Esther Bulaya (Bunda Mjini), Joseph Mbilinyi (Mbeya Mjini) na wa Viti Maalumu Mariam Msabaha.

Aidha, alisema Chadema imetuma ujumbe wa viongozi wa Kamati Kuu Dodoma kuzungumza na wabunge wao kuhusu Muswada wa Huduma za Vyombo vya Habari ambao unatarajiwa kuwasilishwa bungeni na Serikali.

Alitaja wajumbe wa Kamati Kuu waliokwenda Dodoma kuwa ni Makamu Mwenyekiti Bara, Profesa Abdallah Safari, Profesa Mwesiga Baregu, Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, Waziri Mkuu mstaafu Fredrick Sumaye na Arcado Ntagazwa.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo