Kesi ya kusambaza matokeo kubadilishiwa hati


Grace Gurisha

Mahakama ya Kisutu
HAKIMU Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, Respecious Mwijage, ameutaka upande wa Jamhuri kubadilisha hati ya mashitaka katika kesi ya kusambaza matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana, kabla ya kuthibitishwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Kesi hiyo inakabili wafuasi wa Chadema na raia wa kigeni na lengo la mwito wa Hakimu Mwijage ni kumwondoa kwenye orodha mshitakiwa aliyefariki ndunia.

Mwijage alifikia uamuzi huo jana na kuahirisha kesi hiyo, baada ya kubaini kuwa katika hati ya mashitaka kuna washitakiwa wanane, wakati kwenye nyaraka za maelezo ya awali, zinatambulisha washitakiwa saba hali ambayo alihofia inaweza kuleta matatizo baadaye.

Kutokana na kubainika kwa makosa hayo, mawakili wa Serikali Grace Komba na Estazia Martin walishindwa kuwasomea washitakiwa maelezo yao.

Kabla ya Hakimu kutoa tarehe ya washitakiwa hao kusomewa maelezo hayo, mawakili wa utetezi, Tundu Lissu na Peter Kibatala walikubaliana na uamuzi huo wa kwenda kubadilishwa hati ya mashitaka.

Kesi hiyo iliahirishwa hadi kesho washitakiwa watakaposomewa maelezo yao. Hatua hiyo inatokana na Jose Nimi (51) raia wa Ufaransa kufariki dunia.

Washitakiwa wengine ni Mashinda Mtei (49) wa Tengeru, Arusha, Julius Mwita (40) wa Magomeni, Dar es Salaam, Frederick Fussi (25) wa Mbezi, Dar es Salaam, Julius Matei (45) wa Kenya, Meshack Mlawa (25) mchungaji wa Keko na Anisa Rulanyan (41) wa Kawe.

Katika kesi hiyo ya mwaka jana yenye mashitaka matatu wanakabiliwa na madai ya kutoa taarifa za uongo kwenye mitandao wakati wakijua hazijathibitishwa.

Ilidaiwa kuwa Matei na Nimi, Oktoba 26 mwaka jana wakiwa kwenye hoteli ya King, Kinondoni wakiwa na hati za kusafiria namba A1532119, 930879 na M 27687807 walijiingiza kwenye ajira ya kukusanya na kusambaza matokeo ya urais ya uchaguzi wa mwaka jana ya Chadema bila kibali.

Mashitaka la ya tatu yanamkabili Matei peke yake mwenye hati ya kusafirilia namba A1532119 ambaye inadaiwa akiwa Dar es Salaam alijihusisha na biashara kwenye Saccos ya Wanama bila kibali.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo