Watakiwa kutoa takwimu sahihi


Enlesy Mbegalo

Profesa Innocent Ngalinda
WAKUSANYA takwimu wametakiwa kutoa takwimu sahihi ili kuiwezesha Serikali kupanga mipango yake.

Hayo yalisemwa jana Dar es Salaam na Mkuu wa Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika, Profesa Innocent Ngalinda alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu mafunzo ya wakusanya takwimu yaliyoanza Oktoba 17.

Profesa Ngalinda alisema ili kuhakikisha ubora wa takwimu unazingatiwa na kulingana na matakwa ya kiutendaji ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), ni lazima anayefanya awe amepitia chuo hicho.

“Takwimu ni taaluma kama nyingine ukikosea Serikali itashindwa kupanga maendeleo ya baadaye na ili kuondokana na mazoea ya ukusanyaji taarifa, tumeaza kutoa mafunzo hayo ili kupunguza gharama za ukusanya takwimu,” alisema Profesa Ndalinda.

Alisema mafunzo hayo yaliandaliwa ili kumpa mshiriki ujuzi katika ukusanyaji takwimu kwenye mazingira mbalimbali kwa ajili ya kuzichakata na kuwa takwimu rasmi.

“Nashauri umma kuchangamkia fursa ya mafunzo haya kwa sababu uhitaji wa wakusanya takwimu wenye ujuzi unakua,” alisema.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo