Wanafunzi 1,780 UDSM, IMF wakopeshwa


Hussein Ndubikile

WANAFUNZI 1,780 wa mwaka wa kwanza wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), wamepewa mikopo na Serikali.

Hatua hiyo imekuja baada Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa juzi kutangaza kuwa hadi leo asilimia 90 ya wanafunzi wa elimu ya juu wanaostahili mikopo watakuwa wamepata.

Kwa mujibu wa Serikali UDSM ina wanafunzi 3,666 wa mwaka wa kwanza wanaostahili mikopo, huku IFM ikiwa na wanafunzi 2,000. 

Wakizungumza na JAMBO LEO kwa nyakati tofauti viongozi wa Serikali za wanafunzi wa vyuo hivyo walisema Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) juzi ilianza kupeleka majina ya wanafunzi wanaopata mikopo huku wakisitiza kuwa kitakachofuata ni mchakato wa kusainisha wanafunzi hao.

Waziri Mkuu wa Serikali ya Wanafunzi wa UDSM (Daruso), Boniphace Emmanuel alisema Ijumaa iliyopita Bodi hiyo ilipeleka majina 646 ya wanafunzi huku jana yakipelekwa mengine 900 na kufanya idadi kuwa 1,546.

Alisema wanafunzi wapatao 11,000 wanaoendelea na masomo ya shahada mbalimbali bado majina yao hayajawasilishwa chuoni hapo na walipojaribu kufuatilia, waliambiwa suala lao linashughulikiwa na Bodi.

Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa IFM (IFM-SO), Kilonzo Mringo alisema kabla Waziri Mkuu hajatoa tamko lake, Bodi ya Mikopo ilishapeleka majina 240 huku akiongeza kuwa walishauri wanafunzi wasisaini mpaka watapojua hatima ya majina ambayo hayajapelekwa.

Alisisitiza kuwa wanafunzi 2,864 wa mwaka wa pili na wa tatu   majina yao hayajapelekwa hali inayofanya waliofika kuanza muhula kuishi kwa tabu huku wanaotoka mikoani wakisita kuripoti kukwepa ukata huo.

Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo