Askofu aifunda CCM


Abraham Ntambara

William Mwamalanga
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimetakiwa kuacha vita ya maneno na vyama vya upinzani, badala yake wamsaidie Rais katika kutatua changamoto zinazowakabili wananchi.

Hayo yalielezwa na Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kipentekoste Tanzania, William Mwamalanga alipozungumza jana na JAMBO LEO.

Askofu Mwamalanga alisema CCM wanapaswa kuchapa kazi na siyo kuchonga maneno na wapinzani.

“CCM wanapenda malumbano na vyama vya upinzani kiasi cha kila kukicha wanatafuta sababu kwa kufanya malumbano hayo,” alisema Mwamalanga.

Mwamalanga alisema kwamba CCM, wanashindwa kumsaidia Rais mambo mengi na hawajui kama kuendeleza malumbano hayo ni dalili ya kushindwa kuisaidia serikali yao katika kutekeleza majukumu.

Alifafanua kuwa chama tawala ndiyo msaidizi wa Rais kwa mambo ya ushauri, kutatua kero za wanyonge na misaada kwa wananchi wahitaji badala yake kimekuwa hakifanyi hivyo na nidhahiri hakipo karibu na wananchi wanyonge.

Alisema CCM wanatakiwa si kila suala linalozungumzwa na wapinzani na wao waibuke na kuwajibu inatakiwa watambue kuwa uchaguzi ulikwisha hivyo watekeleze ahadi zao za kwenye Irani yao ya uchaguzi huku wakiwasubiri wapinzani kupambana nao katika uchaguzi ujao wa mwaka 2020.

Alisesitiza kwamba chama tawala kinatakiwa kupambana katika kuwajibika kwenye kazi ili wawadehihirishie wananchi na wapinzani kwa uchapakazi wao kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.

Askofu Mwamalanga alibainisha maisha ya watu kwa hivi sasa nchini wanahali mbaya kutokana na ugumu wa kiuchumi unaowakabili hivyo ingetegemewa kuona ni namna gani serikli inatoa majibu juu ya hali hii kwa wananchi.

Aidha aliwataka watambue kuwa viongozi wa vyama vya upinzani wanafanya wanapowasema wanakuwa na lengo la kuwachokoza ili washindwe kufanya kazi na hivyo kuingia katika mtego wao na kulumbana wakati wananchi siyo hitaji lao.

Alisema hivi sasa watu wanaona Rais yuko peke yake na hakuna wanaomsaidia ambao aliongeza hadi leo watu wanalalamika kwa nini rais hajafika Kagera ambapo alifafanua kuwa hayo ndiyo yanegekuwa masuala ya kuzungumza kwenye chama.

Mwamalanga alisema ingetegemewa Katibu Mkuu, Msemaji na viongozi wengeine wa chama wangekuwa huko Kagera kama chama tawala kikiongoza katika misaada ku badala yake hawajafanya chochote wamemuachia Mkuu wa mkoa tu.

Alisema Kama viongozi wa dini wameona suala hilo siyo sahihi ambapo wamewataka CCM kama chama tawala kuwa mstari wa mbele katika utekelezaji wa maagizo ya Rais.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo