Mkataba bomba la mafuta wasainiwa


Mariam Cyprian, Tanga

Profesa Sospeter Muhongo
SERIKALI za Tanzania na Uganda zimesaini mkataba wa utekelezaji mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi unaotarajiwa kuanza hivi karibuni kutoka Ziwa Albert hadi bandari ya Tanga.

Mkataba huo ulisainiwa juzi baada ya kikao cha siku tatu kati Tanzania na Uganda kilichofanyika mkoani hapa.

Makataba huo ulisainiwa na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo na mwenzakde wa Uganda, Irene Muloni.

Akizungumza baada ya kusaini mkataba huo, Profesa Muhongo alisema mkataba umegusa maeneo mbali mbali muhimu yakiwamo ya upatikanaji ardhi, ulinzi na uwekezaji.

Profesa alisema serikali hizo zinashirikiana kwa ukaribu kuhakikiasha mradi huo unakamilika kwa wakati na kuanza kufanya kazi mwaka 2020.

"Mradi upo na kasi ya utekelezaji ipo lengo ni kuhakikisha ifikapo mwaka 2020 mradi unakamilika na sasa ni wakati wa kila mtu kuwa tayari kwa ajili ya mradi huo," aliongeza Muhongo.

Waziri Muloni alisema alifurahi kuona jinsi wananchi wa nchi hizo walivyo na shauku ya kuupokea mradi huo.

"Jana (juzi) nilitembelea maeneo mbalimbali ya Tanga ikiwamo bandari sehemu ambayo bomba la mafuta litapita na niliona ni jinsi wananchi wanavyoufurahia mradi huu, hivyo ni wakati sasa wa kufanya kazi na wananchi, wajiandae," alisema Muloni.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo