JPM ataka Kenya, Tanzania kujadili usalama


Enlesy Mbegalo

Rais John Magufuli
RAIS John Magufuli ametaka mawaziri wa Mambo ya Nje wa Kenya na Tanzania kukutana kabla ya mwisho wa mwaka huu kujadili usalama wa nchi hizo, huku akitaka wafanyabiashara wa Kenya kuja kuwekeza nchini.

Kwa mujibu wa taarifa ya Kurugenzi ya Mwasiliano ya Rais Ikulu kutoka Kenya, Rais Magufuli alisema kutokana na ujirani uliopo kati ya nchi hizo, ni lazima usalama uimarishwe.

“Ni lazima mawaziri wa Kenya na Tanzania wakutane kabla ya mwaka huu kwisha ili wajadili mambo ya usalama wa nchi hizi,” alisema Rais Magufuli.

Alisema ziara hiyo inampa fursa ya kujenga upya uhusiano wa Tanzania na Kenya katika nyanja mbalimbali ikiwamo kuimarisha biashara kati ya mataifa hayo mawili.

“Hii ni kuthibitisha kuwa Watanzania na Wakenya ni ndugu mfano Kenya kuna Wamasai na Tanzania wapo pia lakini wanapotaka kulisha mifugo yao lazima waangalie mipaka,” alisema Dk Magufuli

Aliwataka Wakenya kuwekeza biashara zao Tanzania kwa lengo la kukuza uchumi wa nchi hizo.

“Nchi ya kwanza ya kiafrika yenye uwekezaji mkubwa Tanzania ni Kenya, hakuna nchi nyingine ya kiafrika zaidi ya hii,” alisema.

Alisema Kenya ni nchi rafiki namba moja katika Afrika ambayo imewekeza zaidi ya kampuni 526 kwa wastani wa dola za bilioni 1.7 za Marekani.

“Kampuni hizo zimeajiri Watanzania 59,260. Takwimu hizi zinaifanya Kenya kuwa nchi ya kwanza ya kiafrika yenye uwekezaji mkubwa nchini,” alisema Rais Magufuli.

Aliongeza kuwa jumla ya thamani ya biashara kati ya Tanzania na Kenya imeongezeka kutoka Sh bilioni 600 mwaka 2010 hadi Sh trilioni 2. 044 mwanzoni mwa mwaka huu.

Rais Uhuru Kenyatta alitaja suala ya mawasiliano kuwa ni moja ya watakayoshirikiana na kwamba mawaziri wa mambo ya nje wa Kenya na Tanzania watakutana kupanga mambo ya majeshi, kuimarisha usalama.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo