Lipumba asisitiza Mwenyekiti halali CUF


Sijawa Omary, Mtwara

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi, (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba amerudia kueleza sababu za uamuzi wake kujiuzulu uenyekiti wakati wa mchakato wa Uchaguzi Mkuu mwaka jana.

Amesema ukiukwaji wa Katiba ya CUF kwenye baadhi ya mambo ilimchefua na kulazimika kufanya uamuzi huo mgumu katika kipindi kigumu, lakini akasema hadi sasa yeye ndiye Mwenyekiti halali wa CUF, akitaka wanaCUF kudharau mambo aliyoyaita ya uzushi kuhusu chama hicho na yeye kwenye mtandao.

Alisema hayo jana mjini hapa alipozungumza na wanachama wa katika kikao cha ndani akiwa katika ziara ya siku mbili kabla ya kwenda Lindi kuendelea na ziara hiyo.

“Ndugu zangu wanachama, nimetengua rasmi uamuzi huo wa kujiuzulu baada ya kupandwa na jazba kutokana na uvunjwaji wa Katiba yetu, sasa tuendelee kujenga chama chetu kwani nimerudi. Mimi niko ngangari kinoma, msiamini mambo ya kwenye mitandao niko ngangari,” alisema Lipumba.

“Msimamo na Mwongozo wangu Profesa Ibahim Lipumba ni Mwenyekiti halali wa CUF na mwanachama halali na huu ni msimamo na mwongozo ambao umesimamia Katiba yetu kwani haki ya kujiuzulu ninayo na ya kutengua ninayo, hapakuwa na sababu ya kufika hapa,” alisema.

Alipongeza wanachama wa jimbo la Mtwara Mjini kwa moyo waliouonesha hasa katika kukiweka chama hicho kushika madaraka kwenye jimbo hilo.

Alisema lengo la ziara hiyo ni kuijenga na kuiimarisha CUF Tanzania Bara ambapo alisema jambo muhimu kwa wanaCUF na viongozi ni kuhakikisha wanaendelea kuijenga ili izidi kupata heshima.

“Mlionesha uamuzi sahihi kuhakikisha CUF inashika madaraka Mtwara kuanzia jimbo na halmashauri kwa jumla, hongereni sana kwa hili, mmeonesha uimara wa chama chetu tena kwa ushindi mkubwa, hongereni kwa kazi nzuri,” alisema Lipumba.

Mwenyekiti huyo aliyefuatana na mbunge wa Mtwara Mjini, Maftaha Nachuma alifungua matawi mawili ya CUF katika kata za Magomeni na Ufukoni, ambako pia alitaka wanachama kukilinda na kukikuza chama hicho ili kizidi kuwa imara.

Mbunge Nachuma aliwahakikishia wapiga kura hao kwa tuhuma zilizoripotiwa na vyombo vya habari kuwa amesimamishwa uanachama jambo ambalo si sahihi na kwamba yeye atakuwa wa mwisho kurudisha kadi ya chama hicho.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo