Ndugai ashangaa wanaomchukia


Joyce Kasiki, Dodoma

MBUNGE wa Kongwa, Job Ndugai (CCM), amewatolea uvuvi watumishi wa Halmsahuri ya Wilaya ya Kongwa wanaomchukia akisema haoni sababu kwa watumishi hao kumchukia.

Akizungumza kwenye Kikao cha Baraza la Madiwani wa halmshauri hiyo, Ndugai alisema licha ya yeye kuwa mstaarabu miongoni mwa wabunge wa sasa, anashangaa chuki dhidi yake akihoji inatoka wapi. 

Kabla hicho kilichofanyika mwishoni mwa wiki Ndugai ambaye pia ni Spika wa Bunge, alikuwa hajawahi kuhudhuria vikao vya baraza hilo tangu aliporejea kutoka nchini India kwa matibabu.

"Namshukuru Mungu kwa sababu halikuwa tarajio langu kama ningeweza kuiona siku hii miezi machache iliyopita, nimepita katika mazingira magumu, nilikuwa na hali ngumu kiafya…; wapo waliofurahi, wengine walisikitika, lakini nimepata nafasi ya kujua binadamu wakoje.
Kwa waliofurahi nilijiuliza maswali, hivi kumbe mimi kumbe ni mzigo, lakini nikajiuliza  kama  ni mzigo ni kwa kipi,  sioni sababu ya kunichukia, lakini ukweli utabakia pale pale kwamba tuishi vizuri na tusaidiane," alisema.

Aliwataka madiwani na watumishi wa halamshauri hiyo kushirikiana katika utendaji kazi na kutoa ushirikiano kwa mkurugenzi wa halamshauri hiyo na Mkuu wa Wilaya ya Kongwa ambao ni watumishi wapya ili Kongwa iendelee kustawi kimaendeleo.

"Naomba tusiwaingize hawa wakuu wetu katika zile mila na destur zetu za uongo,kudanganya,mtu unataka DC (Mkuu wa Wilaya),  apigane vita yako kwa sababu tu wewe una ajenda zako,tuachane na hayo haisaidii hakmashauri,tuangalie suala la maendeleo zaidi," alisema

Amewataka viongozi na watumishi wote kufanya kazi kwa uadilifu ili kuepuka adha ya kutumbuliwa kwa kutofuata maadili ya kazi zao.

"Usitegemee kwa sababu wewe ni Diwani ukaenda kujenga daraja, zahanati ukaweka mrija wako pale ili uishi, hizo enzi zimepita, awamu hii ikiletwa hela fulani  kufanya kazi ya Serikali hiyo ni ya Serikali, enzi  zile za kujineemesha mwenyewe kwa ujanja ujanja zimepita, maana wananchi walchagua mabadiliko na haya ndio mabadiliko yenyewe," alionya Ndugai

Alisema anaamini Serikali inaendelea kujenga miundombinu mbalimbali kwa ajili ya kusogea huduma karibu na wananchi hususan miundombinu ya umeme.


Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo