ACT Wazalendo wataka Rais aheshimu Katiba ya Warioba


Mwandishi Wetu

CHAMA cha ACT Wazalendo kimetaka mchakato wa kuandika Katiba Mpya uanze kwa kufanya Marekebisho ya Sheria ya Kura ya Maoni, kikimshauri Rais John Magufulikuunda timu ya wataalamu, kupitia Rasimu ya Katiba ya Jaji Joseph Warioba, kuitisha mkutano wa kikatiba ili kupitisha Katiba Pendekezwa hadi kufikia hatua ya Kura za Maoni

Kwa mujibu wa maazimio yaliyofikiwa na mkutano wa kwanza wa kisera wa chama hicho tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu, ACT imesema kuna umuhimu wa marekebisho kwa sheria hizo na ile ya Mchakato wa Katiba kwa muastakabali wa Taifa.

Chama hicho pia kimetaka kujalidiwa kwa Azimio la Arusha katika miaka 25 ya kutekelezwa kwake na madhara yake tangu lilipozikwa visiwani Zanzibar mwaka 1992.

“Chama kimeazimia mchakato wa kuandika Katiba Mpya uanze kwa kufanya marekebisho ya Sheria ya Kura ya Maoni na Sheria ya Mchakato wa Katiba,” ilisomeka sehemu ya maazimio hayo.

Kwa mujibu wa maazimio hayo iwapo Serikali itaamua kwenda na Katiba Pendekezwa iliyopo sasa, ACT itaipinga kwa kufanya kampeni za HAPANA kwenye kura ya maoni.

Kwa mujibu wa ACT, wakati mchakato wa Katiba ukiwa umesimama Baraza la Wawakilishi la Zanzibar limepitisha Sheria ya Kutafuta Mafuta na Gesi kinyume na matakwa ya Katiba ya Muungano inayoeleza mafuta na gesi ni masuala ya Muungano.

Mkutano Mkuu wa Kidemokrasia ACT pia umeshauri mbunge wake, Zitto Kabwe ambaye pia ni kiongozi wa chama hicho kuwasilisha muswada binafsi wa Mabadiliko ya Katiba ya Muungano yanayolenga kuondoa mafuta na gesi kwenye mambo ya Muungano.

Kwa mujibu wa maazimio hayo ya ACT, kufanya hivyo kutaiwezesha Zanzibar kuendelea na utafutaji na uchimbaji wamafuta na gesi asilia bila vikwazo vya kiufundi kwa ajili ya kikatiba.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo