Wosia wa Rais waibua mjadala mitandao ya kijamii


Fidelis Butahe

UTANI uliotolewa juzi na Rais John Magufuli kuhusu idadi tofauti ya wake wa aliyekuwa Meya wa Jiji Dar es Salaam, marehemu Didas Masaburi umeibua mjadala mkali katika mitandao ya kijamii.

Watu wa kada mbalimbali walitoa maoni yao katika mitandao ya Twitter, facebook na Instagram waliungana na mkuu huyo wa nchi kwa maelezo kuwa utani huo huenda ukamaliza mpasuko wa familia ya marehemu, wengine wakitofautiana naye kwa madai kuwa utaleta vurugu zaidi.

Kauli hiyo ya Rais iliibua vicheko, minong’ono na mjadala miongoni mwa mamia ya waombolezaji waliojitokeza kuaga mwili wa Masaburi aliyefariki Jumatano iliyopita, wale waliokuwa na nyuso za huzuni, ghafla walianza kutabasamu na kumpigia makofi.

Rais huyo wa Awamu ya Tano alitoa kauli hiyo baada ya mdogo wa marehemu, Joackim Machabe kusoma wasifu ambao pamoja na mambo mengine, alisema kaka yake alifunga ndoa na Janeth Masaburi, lakini ameacha wajane, watoto 20 na wajukuu kadhaa.

Katika ufafanuzi wake, Rais alisema marehemu alikuwa na wake wanne au watano na watoto zaidi ya 20, huku akiwataka watoto hao kushikamana huku akitumia Biblia Takatifu kutoa mfano wa mfalme Suleiman aliyekuwa na wake na watoto wengi.

Katika mtandao wa facebook, Rehema Msami alisema, “baada ya kusikia mtu akitumia maandiko ya Suleiman kuwa na wake wengi ili kuhalalisha uovu…, nilitamanai mtu huyo angetumia maandiko ya Suleiman alipoomba hekima kutoka kwa Mungu,” alisema.

Katika moja ya mijadala iliyoibuliwa katika mtandao wa facebook kuhusu suala hilo, Ruth Kowero aliandika, “kufa ni kufa na kila mtu atakufa na ukweli utabaki pale pale, alichokifanya Rais ni nafuu kwa familia.”
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo