Wenye ulemavu wa kusikia wamtaka JPM

Mariam Cyprian, Tanga

Dk John Magufuli
WATU wenye ulemavu wa kusikia mkoani hapa wamemwomba Rais John Magufuli kutembelea makundi ya walemavu wa aina zote ili kutambua changamoto zao na kuzipatia ufumbuzi.

Akizungumza jana Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Viziwi Tanzania (CHAVITA) Mkoa wa Tanga, David Nyange alisema makundi hayo yamesahaulika na kukosa nafasi za ajira na ruzuku za Serikali. 

Alisema Chavita imesahaulika licha ya kutambuliwa na Serikali na kumtaka Rais awatembelee kujua namna wanavyokabiliana na changamoto za ukosefu wa ajira na kusababisha kutegemea wafadhili   kuendesha maisha yao.

Nyange alisema walemavu wengi wanakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa ajira kwa kudharauliwa kwenye halmashauri kutokana na mtizamo hasi ambao unasababisha kuonekana wao si kitu kwenye jamii hivyo kushindwa kupata ajira hususan kwenye taasisi za umma na binafsi.

‘’Tunamwomba Rais wetu atembelee makundi ya watu maalumu wenye ulemavu wa kutosikia, ili wamweleze atunge sheria yenye meno makali itakayotulinda na kuhakikisha tunapata ajira na mikopo ikiwamo ruzuku kama watu wengine,” alisema Nyange.

Akifafanua kuhusu ukosefu wa ajira kwa makundi ya watu wenye ulemavu wa kutosikia, Katibu wa CHAVITA Tanga, Monalisa Athumani alisema makundi hayo hayapewi kipaumbele ipasavyo kutokana na mitazamo hasi inayoendelea kuwa donda sugu hivyo kushindwa kunufaika na rasilimali zao na maisha kuwa magumu.

“Makundi ya walemavu hususan viziwi, tumesahaulika sana hali inayofanya kushindwa kupiga hatua kimaendeleo kwa kukosa fedha na mafungu kwenye halmashauri, licha ya kupata ushirikiano lakini huduma zinazohusu makundi hayo kwenye mfuko wa maendeleo ya jamii hatuzipati,” alisema Nyange.

Aidha, Katibu huyo alilalamikia Serikali kushindwa kutenga fedha na kuyapa ruzuku makundi ya wenye ulemavu wasiosikia hali inayosababisha makundi hayo kunyanyasika na kuwa ombaomba mitaani.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo