Brela yataka vijana wawe wabunifu


Mwandishi wetu, Dar es Salaam

Andrew Mkapa
WAKALA wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela) umetoa wito kwa vijana nchini kutumia fursa mbalimbali za mafunzo ya ujasiriamali na biashara ili kujijengea uwezo wa kujiamini wanapoamua kujiingiza katika biashara.

Naibu Msajili wa Wakala (Sheria za Biashara), Andrew Mkapa, amesema kuwa mafunzo ya ujasiriamali na biashara ni nguzo muhimu kwa vijana, hasa wanapokuwa na malengo ya kujiajiri kwani mafunzo hayo hutoa mwongozo.

“Nawashauri vijana kujitokeza kwenye mafunzo ya ujasiriamali na biashara ili muweze kujijengea uwezo na kujua umuhimu wa kurasimisha biashara zenu ili mtambulike na mamlaka husika,” alisema

Mkapa alitoa wito huo mwishoni mwa wiki, baada ya kutoa mada kwenye semina ya ujasiriamali kwa vijana iliyoandaliwa na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ali Hapi kwa lengo la kuwajengea vijana uwezo wa kujiajiri.

Mkapa aliwataka vijana kuondokana na dhana ya kusubiri kuajiliwa pindi wanapomaliza shule badala yake wajikite zaidi kwenye kujiajiri wenyewe kwenye biashara na shughuli nyingine za kijamii.

“BRELA imeamua kujikita zaidi katika kutoa elimu ya mafunzo ya kurasimisha biashara kwa vijana ili kuwahamasisha wapate ufahamu wa namna ya kuanzisha kampuni na majina ya biashara ili waweze kutambulika kisheria,” alisisitiza.

Mkapa ambaye pia alitoa mada iliyowasisimua zaidi vijana, alimpongeza DC Hapi kwa jitihada za kuwakutanisha vijana pamoja na kutoa mafuzo ya ujasiriamali na biashara.

“Kwa niaba ya Ofisa Mtendaji Mkuu na Msajili wa Kampuni, nachukua fursa kumpongeza mkuu wa wilaya, wawezeshaji na washiriki wote kwenye mafunzo haya,” alisema na kuongeza kuwa Brela ipo tayari muda wote kutoa elimu jinsi ya ya kusajili makampuni, jinsi ya kusajili majina ya biashara na faida zake.

Haya mafunzo yana maana na yatawasaidia sana vijana pindi watakapoanza kuunganishwa na fursa mbalimbali zinazotolewa kama vile ya mikopo kwani tayari watakuwa na uwelewa mkubwa wa kuzitumia fursa.

“sio tu kwa vijana hawa waliohudhuria leo hapa lakini ni kwa watu wote kwa ujumla nchi nzima ni muhimu katika karne hii ya sasa kufanya biashara zilizo rasmi,” alisisitiza Mkapa

Mshiriki wa mafunzo, Bw. Medson Moshi ni miongoni mwa vijana waliohudhuria semina hiyo na aliwataka na kuwahimiza vijana wengine kuchangamkia fursa kama hizo na kuachana na mtazamo wa kusubiri kulipwa fedha ili kuweza kudhuria semina za mafunzo kama hiyo.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo