Akumbushia nyumba aliyoahidiwa na Nyerere


Salha Mohamed

Mwalimu Julius Nyerere
ASKARI mstaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Mwanahamisi Musa amelalamika kutotimiziwa ahadi ya kujengewa nyumba aliyoahidiwa na Baba wa Taifa, marehemu Mwalimu Julius Nyerere.

Mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam aliyekuwa ziarani Pugu Stesheni mkoani humo juzi, Mwanahamisi anayekadiriwa kuwa na umri wa zaidi ya miaka 80 aliyestaafu Jeshi mwaka 1984, alisema alipewa ahadi hiyo kwa kuwa mwanamke wa kwanza wa JWTZ kufanya kazi kwenye kitengo cha Rada za kuongozea ndege nchini, hivyo kuandika historia.

Alidai kuwa kutokana na nafasi hiyo, Mwalimu Nyerere wakati huo akiwa Rais, alimwahidi nyumba kama shukrani za kutambua mchango wake.

”Niliahidiwa na Nyerere kujengewa nyumba kwa sababu nilikuwa mwanamke wa kwanza kusimamia Rada, lakini nasikitika ahadi ya mzee… nasikia uchungu…kwa nini Mungu alimchukua kabla hajanikamilishia ahadi yangu!” Alilalamika Mwanahamisi.

Alifafanua kwamba ahadi ya Baba wa Taifa ilieleza kiuwa nyumba hiyo  angejengewa  nyumbani kwao Tabora na tayari alikuwa na eneo la ujenzi alilopewa na Idara ya Ardhi ambalo hata hivyo, liliporwa na kuuziwa mtu mwingine ambaye pia ameliuza.

Akijibu hoja ya Mwanahamisi, Makonda alisema Rais John Magufuli anathamini michango ya wazee waliotumikia Taifa hili pamoja na  Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange kuwa ni msikivu.

“Ikibainika ni kweli uliahidiwa kujengewa nyumba hiyo na kuwa wewe ulikuwa mtumishi wa JWTZ tena mwanamke wa kwanza kufanya kazi katika kitengo muhimu cha Rada, mimi nitakutafutia kiwanja Tabora  na nitakujengea nyumba ya vyumba vitatu Tabora,” alisema Makonda na  mstaafu huyo kumshukuru.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo