Maghorofa 5 kujengwa Magomeni Kota


Mwandishi Wetu

WAKALA wa Majengo Tanzania (TBA) unatarajia kujenga maghorofa matano ya ghorofa nane hadi tisa kila moja katika awamu ya kwanza ya ujenzi wa nyumba za makazi Magomeni Kota, Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Ushauri wa TBA, Edwin Nnunduma alisema hayo jana wakati wa ziara ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kukagua ujenzi huo katika eneo hilo.

Awali Majaliwa alitaka wataalamu wa ujenzi wa mradi wa nyumba za makazi Magomeni watumie utaalamu wao vizuri wakamilishe ujenzi huo kwa wakati.

Waziri Mkuu alitaka wataalamu hao waendelee kufanya kazi hiyo kwa kufuata misingi ya weledi wa taaluma yao, kwani Serikali inawaamini.

“Muhimu mjue kwamba mmepewa dhamana hii kubwa ya kukamilisha ujenzi huu, ili wananchi waliokuwa wanaishi hapa warudi kwenye makazi yao,” alisema.

Nnunduma katika maelezo yake, alifafanua kuwa awamu ya kwanza ya ujenzi huo itahusisha majengo matano.

“Kati ya majengo haya, manne yatakuwa na ghorofa nane na moja   ghorofa tisa, ambapo wakazi zaidi ya 600 waliokuwa eneo hili tangu zamani watakabidhiwa,” alisema.

Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo