Kamanda wa Polisi Singida afariki


Hussein Ndubikile

Peter Kakamba
KAMANDA wa Polisi wa Mkoa wa Singida, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP), Peter Kakamba, amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), alikokuwa akipata matibabu.

Taarifa iliyotumwa jana kwenye vyombo vya habari na Msemaji wa Jeshi hilo, Advera Bulimba, ilieza kuwa Kamanda huyo alifariki dunia alfajiri ya kuamkia juzi.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa Kakamba alijiunga na Jeshi hilo mwaka 1988 na kupanda vyeo mbalimbali vikiwamo vya konstebo (1988), Sajini (1991), Mkaguzi Msaidizi (1997) na Mkaguzi (2003).

Alipanda kuwa Mrakibu wa Msaidizi (2006), Mrakibu (2008), Mrakibu Mwandamizi (2011) na Kamishna Msaidizi (2015).

Alisema Kakamba aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali zikiwamo za Mwendesha Mashitaka wa Mkoa wa Iringa, Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Mufindi, Ofisa Mnadhimu wa Polisi mikoa ya Iringa na Geita na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa.

Alizaliwa mwaka 1963 katika kijiji cha Kawajense, Mpanda mkoani Katavi na kupata elimu ya msingi kwenye shule ya Shanwe, Kawajense (1973-1980) na kidato cha kwanza hadi cha nne sekondari ya Kantalamba (1981-1984).

Alipata elimu ya vidato vya tano na sita sekondari ya Umbwe, Kilimanjaro (1985-1987) na Astashahada ya Sheria ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (1992-1994).

Mkuu wa Jeshi Polisi nchini (IGP), Ernest Mangu alitoa pole kwa maofisa, wakaguzi, askari, ndugu, jamaa na marafiki waliofikwa na msiba huo.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo