DCI wa zamani awa Katibu Tawala Kagera

Mwandishi Wetu

Diwani Athuman
RAIS John Magufuli amemteua aliyekuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Diwani Athuman, kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera.

Taarifa ya Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa iliyotumwa kwa vyombo vya habari jana, ilieleza kuwa uteuzi wa Athuman unaanza mara moja.

Mwishoni mwa mwezi uliopita, Rais Magufuli alitengua uteuzi wa Athuman katika nafasi yake ya DCI, katika taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi, bila kueleza sababu.

Kijazi katika taarifa hiyo, alisema Athuman aliteuliwa kushika nafasi hiyo Mei mwaka jana, akitokea nafasi ya Kaimu Kamishna wa Kamisheni ya Intelijensia ya Jinai, atapangiwa kazi nyingine na uteuzi wa Mkurugenzi mpya wa Makosa ya Jinai utatangazwa baadaye.

Mbali na uteuzi huo, Rais Magufuli pia alifanya uteuzi wa wenyeviti wa bodi za taasisi tano za Serikali, ambapo aliyekuwa Waziri Mkuu, Jaji Joseph Warioba, aliteuliwa kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA).

Kwa mujibu wa taarifa ya Msigwa, uteuzi wa Jaji Warioba aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba katika Serikali ya Awamu ya Nne, ulianza Jumatano.

Uteuzi mwingine uliofanyika ni wa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), nafasi aliykabidhiwa Dk Jones Kilimbe, huku aliyekuwa Mbunge wa Dole na Mwenyekiti wa Bunge, Sylvester Mabumba, akiteuliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya TCRA. Uteuzi huo ulianza juzi.

Bodi nyingine iliyopata uongozi ni ya Shirika la Uhandisi na Usanifu Mitambo (Temdo), ambapo Profesa Patrick Makungu, aliteuliwa kuwa Mwenyekiti katika uteuzi ulioanza Jumatano.

Rais Magufuli pia alimteua Martin Madekwe kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Fidia ya Ardhi katika tangu juzi huku Profesa Raphael Chibunda, akiteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wakurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Viuatilifu vya Kitropiki Tanzania (TPRI).
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo