Samia: Serikali imepiga hatuia kulinda haki


Mwandishi Wetu

Samia Suluhu Hassan
MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali imepiga hatua kulinda na kutetea haki za binadamu kwa kuzingatia maazimio ya ndani na ya kimataifa ikiwamo haki ya kuishi.

Samia alisema hayo jana jijini Arusha wakati akifungua mkutano wa  masuala ya demokrasia na haki za binadamu ya Mahakama ya Afrika ya Watu na Haki za binadamu kwa niaba ya Rais John Magufuli.

Alisema Tanzania ni mfano wa kuigwa Afrika kwa kuzingatia na kutekeleza ipasavyo mikataba ya kimataifa inayolenga kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na za msingi ikiwamo ya afya na elimu bila kubaguliwa.

“Serikali itaendelea kutekeleza na kuzingatia matamko ya dunia yanayolenga kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za kijamii ikiwamo haki ya kuishi,” alisema Samia.

Alisema anafurahishwa na hatua zinazochukuliwa na baadhi ya nchi za Afrika kulinda na kutetea haki za binadamu hasa za wanawake akiongeza kuwa bado kuna umuhimu kwa nchi zinazosuasua kutekeleza mikataba hiyo, kuanza kuitekeleza ili kuhakikisha wanawake na watoto wanapata haki sawa katika jamii.

Alibainisha, kwamba Tanzania imepiga hatua kuingiza wanawake kwenye ngazi za uamuzi na kwa sasa mpango kabambe unaandaliwa kuhakikisha sekta binafsi yenye idadi ndogo ya wanawake kwenye ngazi za muamuzi kufanya hivyo.

“Utafiti uliofanyika nchini unaonesha kuwa wanawake wengi walioingizwa kwenye bodi, zimeongeza ufanisi wa kazi maradufu,” alisema.

Rais wa Mahakama hiyo, Jaji Sylvain Ore alisema mkutano huo ni muhimu kwani unalenga kujadili na kuweka mikakati kuhakikisha nchi za Afrika zinazingatia na kulinda haki za binadamu hasa za wanawake.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo