Mgimwa ahimiza wananchi kutalii


Jemah Makamba

Mahamoud Mgimwa
NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii, Mahamoud Mgimwa ametaka Watanzania wawe na utaratibu wa kutembelea hifadhi na sehemu za vivutio badala ya kuachia wageni peke yao.

Akizungumza Dar es Salaam jana, alisema Watanzania wengi hawana kawaida ya kutembelea vivutio vya ndani ya nchi, jambo ambalo linafanya wageni peke yao ndio waone uzuri wa nchi.

Mgimwa alisema Tanzania ina vivutio vingi na vizuri vyenye kuvutia, lakini Watanzania wanashindwa kutembelea hata sehemu za karibu   na kuachia wageni kufurahia.

Alisema wanatakiwa wawe na kawaida ya kuchanga fedha na mwisho wa mwaka watembelee sehemu tofauti za utalii, kwani bei za kuingia sehemu za utalii ni za kawaida, hivyo wana uwezo wa kumudu na kwenda kuona vivutio na  uzuri wa nchi.

Aidha alisema kuelekea kilele cha Wiki ya Utalii kitakachofanyika Iringa watahamasisha Watanzania wengi, wajifunze kuwa na kawaida ya kujua vivutio na hifadhi za wanyama badala ya kuachia wageni wanaotoka nchi za mbali kuona uzuri wa nchi yao huku wao wakiwa hawajawahi kabisa kutembelea hifadhi yoyote.

Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo