Vodacom yapeleka hisa zake kwa umma


Suleiman Msuya

KAMPUNI ya Mawasiliano ya Simu za Mikononi ya Vodacom, imetangaza dhamira ya kuuza hisa zake kwa umma na baadaye kujiunga kwenye   Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE).

Hatua hiyo ni utekelezaji wa Sheria ya  Elektroniki na Mawasiliano ya Posta (EPOCA) na Sheria ya Fedha ya Mwaka 2016 ambayo inaelekeza makampuni ya simu  kumilikisha  asilimia 25 ya hisa zake kwa wananchi.

Mkurugenzi mkuu wa Vodacom, Ian Ferrao alisema “Tunayo furaha kutangaza kuwa tumeanza rasmi mchakato wa kuuza hisa kwa umma kwa mujibu wa matakwa ya sheria na tumewasilisha maombi na utaratibu mzima utakaotumika kuuza hisa zetu na ratiba yetu nzima,” alisema.

Alisema utaratibu huo utahusu mchakato kwenye Mamlaka ya Usimamiaji wa Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) na DSE.  
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo