‘Ndama Mtoto wa Ng’ombe’ ahoji upelelezi


Grace Gurisha

MFANYABIASHARA maarufu Dar es Salaam Hussein Ndama, maarufu kama ‘Ndama Mtoto wa Ng’ombe (44)’, ameitaka Serikali imweleze upelelezi wa kesi yake utachukua muda gani kukamilika.

Ndama alitaka kujua hilo kwa kupitia Wakili wake, Wabeya Kundya ambaye aliliwasilisha ombi hilo jana mbele ya Hakimu Mkazi, Victoria Ngongwa wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, baada ya Wakili wa Serikali, Christopher Msigwa kudai kuwa upelelezi haujamakilika.

Baada ya kutolewa kwa maelezo hayo, Kundya alidai kuwa ili haki ionekane inatendeka, ni pamoja na kesi kusikilizwa kwa wakati na akaomba kujua upelelezi utachukua muda gani kukamilika, ambapo Msigwa alidai mwathirika mmoja wa tukio hilo, yuko nje ya nchi na ana baadhi ya nyaraka.

Hivyo wanafanya naye mawasiliano ili kuona kama anaweza kuziwasilisha kwa kuzituma au kufika mwenyewe. Kutokana na maelezo hayo, Hakimu Nongwa aliiahirisha kesi hiyo hadi Januari 19.

Mshitakiwa alirudishwa rumande kwa sababu moja kati ya mashitaka yanayomkabili la kutakatisha fedha halina dhamana.

Ndama anadaiwa kuwa Februari 20, 2014 Dar es Salaam, alighushi nyaraka za kibali cha kusafirisha madini na sampuli za madini kwa kusudi la kuonesha kuwa kampuni ya Muru Platnum Tanzania Investment Limited iliruhusiwa kusafirisha makasha manne ya dhahabu yenye kilogramu 207 na thamani ya dola 8,280,000 za Marekani kwenda Australia kwenye kampuni ya Trade TJL DTYL Limited wakati akijua si kweli.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo