Bavicha walia faulo katika uchaguzi mdogo


Mery Kitosio, Arusha

Patrobas Katambi
MWENYEKITI wa Bavicha, Patrobas Katambi, amemtaka Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba kuwachukulia hatua askari ambao wanaenda kinyume na maadili ya utumishi wa umma.

Aliyasema hayo jana katika Ofisi za Makao Makuu ya Chadema mkoani hapa alikokuwa akizungumzia masuala mbalimbali yaliyojitokeza katika uchaguzi mdogo wa udiwani uliokuwa unaendelea katika kata ya Mateves na Ngarenanyuki.

Katambi alidai kuwa katika Kata ya Mateves kumekuwa na uvunjifu wa demokrasia na utawala ambao umekuwa ukitumika katika chaguzi hizo kwa baadhi ya walinzi wa CCM kuwateka na kuwashambulia kwa silaha za jadi vijana wa Chadema ambao walikuwa kwenye maandalizi ya uchaguzi mdogo uliofanyika jana.

"Kumekuwa na uvunjifu mkubwa sana wa misingi ya demokrasia na Utawala wa Sheria kwa maana ya kutoheshimu sheria za nchi zinazoongoza uchaguzi. Juzi katika kata ya Mateves walinzi wa CCM waliwashambuliwa kwa silaha za jadi vijana wa Chadema mbele ya macho ya polisi,” alisema.

Katambi aliwataja vijana watatu walioshambuliwa kwa mapanga na rungu kuwa ni John Mwasele, Joseph Gabriel na Baraka Juma.

Kamanda wa polisi mkoani Arusha, Charless Mkumbo alisema kuwa taarifa ya kukamatwa na kujeruhiwa kwa baadhi ya vijana wa Chadema bado hajazipata ila atazifuatilia kujua chanzo chake.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo