Moi haina uhaba wa vifaa—Msemaji


Emeresiana Athanas

TAASISI ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu Muhimbili (Moi), imesema haina uhaba wa vifaa vya mazoezi ya viungo.

Akizungumza na gazeti hili Dar es Salaam jana, Ofisa Uhusiano wa Moi, Patrick Mvungi alisema taasisi hiyo haina uhaba na kila mgonjwa hupewa matibabu kulingana na mahitaji.

Alisema wataalamu waliopo wanatoa mazoezi ya viungo kwa njia mbalimbali ambazo ni huduma ya mikono kitaalamu na vifaa vya mashine zinazotumia betri.

Mvungi alifafanua kuwa kitengo hicho cha mazoezitiba hakijawahi kurudisha mgonjwa kwa kukosa vifaa, kwani wataalamu wamejifunza njia mbalimbali za kutoa mazoezi kwa wateja wao.

"Tuna vifaa vya kutosha na wataalamu wapo wa kutosha na wanatoa huduma mbalimbali, hatuna uhaba wa vifaa na hatujawahi kurudisha mgonjwa au kuzidiwa kwa kukosa vifaa," alisema.

Mvungi aliwatoa hofu Watanzania na kubainisha kuwa wataalamu hutoa   mazoezitiba kulingana na tatizo la mgonjwa anayefika hospitalini hapo.


Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo