Sekondari 1,629 kupewa vifaa vya maabara


Hussein Ndubikile

Profesa Joyce Ndalichako
WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amsema shule za sekondari zipatazo 1,629 zitagawiwa vifaa vya maabara mwezi huo.

Alisema vifaa hivyo vitagawiwa kwa shule zote ambazo zimekamilisha ujenzi wa maabara, huku akisisitiza shule zinazoendelea na ujenzi huo kukamilisha haraka.

Profesa Joyce Ndalichako alisema hayo katika hafla ya kuzipongeza halmshauri kumi zilizofanya vizuri katika utekelezaji wa mpango wa lipa kulingana na matokeo.

Katika hatua nyingine alizitaka halmashauri zote nchini kuhakikisha zinasimamia vyema upangaji na urekebishaji wa ikama za walimu kwa kuwatawanywa sehemu husika kwa kuzingatia mahitaji ili kuleta tija katika sekta ya elimu.

Alisema sababu kubwa inayosababisha halmashauri nyingi kutofanya vizuri katika sekta hiyo ni upangaji wa walimu usiozingatia mahitaji ya maeneo hali inayozorotesha ufaulu wa wanafunzi.

“Serikali bado haijafurahishwa na halmashauri jinsi zinavyopanga walimu wilayani ndio maana zinashindwa kufanya vizuri kwenye matokeo,” alisema.

Alisema halmashauri zilizoshinda fedha taslimu zilizingatia ufuatiliaji wa suala hilo, uandaaji wa takwimu za shule kwa usahihi pamoja na matumizi sahihi ya ruzuku za uendeshaji wa shule.

Alizitaja halmshauri hizo kuwa ni Wilaya ya Kaliua, Muleba, Geita, Bunda,Rorya, Nzega, Ngara, Itilima, Kongwa na Chato.

Alizigiagiza halmashauri hizo kuzitumia fedha ilizozipata katika urekebishaji wa ikama ya walimu, ujenzi wa madarasa, vyoo na ukamilishaji wa maabara.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo