Zitto atelekeza gari mkutanoni, Polisi yamsaka


Celina Mathew

Zitto Kabwe
JESHI la Polisi Mkoa wa Shinyanga limemtaka Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe, ajitokeze kuchukua gari lake namba T 360 DDV aina ya Toyota Land Cruiser alilolitelekeza uwanjani kwenye mkutano ingawa kuna taarifa kuwa halimiliki kihalali.

Aidha, Jeshi hilo linaendelea kuchunguza kuhusu mmiliki halali wa gari hilo kutokana na taarifa za kiintelijensia kuonesha kuwa Zitto si mmiliki halali na kujitokeza kwa Jaji ambaye hakutajwa jina, aliyedai kumuuzia gari hilo ila hawakukamilisha nyaraka   za mauziano.

Akizungumza na JAMBO LEO jana, Kaimu Kamanda wa Mkoa huo, Elias Mwita alisema Zitto anatakiwa akachukue gari lake na si kama ilivyodaiwa na watu kuwa anatafutwa na Polisi kutokana na uchochezi wa kisiasa.

"Tunamtafuta Zitto ili aje kuchukua gari lake aliloacha hapa wakati wa kampeni ambalo kwa sasa tunaendelea kulichunguza kutokana na kutojulikana mmiliki halali na kwa kuwa Zitto hajaleta vielelezo, hivyo ni vema akavileta ili tujue kama ni lake au la," alisema.

Aliongeza kuwa ni vema akajitokeza ili kurahisisha uchunguzi unaofanywa kuhusu gari hilo ambalo halijulikani mmiliki wake kutokana na kukosekana vielelezo vya umiliki.

Polisi Kahama ambao walichukua gari hilo lililotelekezwa kwenye kampeni walisema baadaye dereva wa Zitto alipoulizwa kama vielelezo vipo alijibu havipo.

"Walilichotaka polisi ni kuletewa vielelezo halali, kwa kuwa siku tulipokuwa tunamtafuta aliliacha uwanjani pale hadi lilipochukuliwa na polisi kwenda kuhifadhiwa hadi mmiliki halali ajitokeze na vielelezo," alisema.

Aidha, Kaimu Kamanda huyo aliliambia gazeti hili jana mchana Zitto aliwasiliana na  Jeshi hilo na kukubaliana kuwa atapeleka vielelezo hivyo ili akabidhiwe gari lake.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo