Mrema ataka sheria ya Parole ibadilishwe


Edith Msuya

Augustino Mrema
MWENYEKITI wa Bodi ya Taifa ya Parole, Augustino Mrema, amesema ni vema sheria ya Parole ikabadilishwa ili wafungwa wote wanufaike nayo.

Mrema alisema hayo jana Dar es Salaam wakati akitoa taarifa ya uzinduzi wa Bodi mpya ya Parole itakayozinduliwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba.

Mrema alisema sheria ya kunufaisha wafungwa ni changamoto kwa Parole ambayo inanufaisha wafungwa wa zaidi ya miaka minne jambo ambalo si zuri.

“Sheria hii ikifanyiwa marekebisho itasaidia kwa kiasi kikubwa wafungwa wengine badala ya wa miaka minne pekee, ili baadaye kupunguza msongamano wa wafungwa magerezani,” alisema.

Alisema mbali na changamoto hiyo, bado Parole inakabiliwa na ukosefu wa fedha hali inayosababisha mchakato wa kuwatoa wafungwa wanaostahili kukwama.

Aliiomba Serikali kuruhusu Bodi hiyo itafute fedha za kufanya mchakato wa Parole kukamilika ili kuwezesha wafungwa wote wanaostahili kutolewa magerezani chini ya sheria ya Parole watoke.

“Naomba mfungwa asiendelee kubaki gerezani wakati anapaswa kutoka chini ya sheria ya Parole na zile Sh milioni 12.8 zilizochangwa na Mchungaji Getrude Lwakatare ni vema zikatumika kukamilisha mchakato wa Parole kwa wafungwa wa Dodoma na mikoa mingine,” alisema.

Hata hivyo, Mrema aliishauri Polisi kuhusu suala la dada poa na mashoga kwamba ni vizuri wakakamata wateja wao.

“Kwani ni uonevu kuwakamata peke yao na kuacha wateja wao ambao ni wanaume kwani dada poa na mashoga ni kikwazo kwenye mapambano dhidi ya Ukimwi,” alisema.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo