JPM ajadili umeme na Rais wa AfDB


Mwandishi Wetu

RAIS John Magufuli amekutana na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), anayeshughulikia nishati, Amadou Hott aliye nchini kwa mazungumzo na wataalamu na viongozi, ili kuboresha sekta ya nishati hususan umeme.

Taarifa ya Ikulu iliyotumwa jana kwa vyombo vya habari, ilieleza kuwa Hott yuko nchini ikiwa ni utekelezaji wa mazungumzo yaliyofanywa kati ya Rais Magufuli na Rais wa AfDB, Akinwumi Adesina jijini Addis Ababa, Ethiopia Januari 31.

Katika mazungumzo hayo, viongozi hao walikubaliana kuongeza ushirikiano kati ya AfDB na Tanzania katika maendeleo, huku mkazo ukielekezwa katika kupata majawabu ya kuongeza uzalishaji umeme wa gharama nafuu.

Hott alielezea kuguswa na dhamira ya Rais Magufuli ya kuongeza uzalishaji umeme wa gharama nafuu, ili kufanikisha mipango ya maendeleo ikiwamo ujenzi wa viwanda na aliahidi Benki yake kuhakikisha dhamira hiyo inafanikiwa.

Rais Magufuli alimhakikishia Hott kuwa Serikali yake iko tayari kutoa ushirikiano wakati wowote itakapohitajika ili kufanikisha dhamira hiyo.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli alizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo nchini, Jean Mutamba Ikulu, Dar es Salaam.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo