Watuhumiwa mauaji ya Mvungi kusomewa ushahidi


Grace Gurisha

Sengodo Mvungi
WAKAZI sita wa Dar es Salaam wanaotuhumiwa kumuua kwa makusudi aliyekuwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dk Sengondo Mvungi, leo wanatarajiwa kusomewa maelezo ya mashahidi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, baada ya upelelezi wa kesi hiyo kukamilika.

Washitakiwa hao ni John Mayunga (56), Juma Kangungu (29), Longishu  Losingo (29), Paulo Mdonondo (30), Mianda Mlewa (40) na Msungwa Matonya (30).

Maelezo hayo yanatarajiwa kusomwa na Wakili wa Serikali, Patrick Mwita mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba wa Mahakama hiyo, ambapo washitakiwa hao waliposomewa mashitaka ya mauaji walikana kuhusika.

Baada ya kusomewa maelezo yao, jalada la kesi hiyo litapelekwa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam ili kesi ianze kusikilizwa, kwa sababu Mahakama ya Kisutu kisheria haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo.

Awali, Mwita aliieleza Mahakama kuwa hawawezi kuwasomea maelezo hayo, kwa sababu bado wanashughulikia taratibu za kuliondoa jina la Chibago Magozi kwenye jalada ambalo lipo Mahakama Kuu, kwa sababu bado hawajapata cheti cha kifo licha ya kuandika barua kwa mamlaka husika.

Awali, washitakiwa walikuwa 11 mmoja akafariki dunia na kubaki 10, na kati yao Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP), Biswalo Mganga aliwasilisha mahakamani nia ya kutoendelea kuwashitaki wanne kwa hiyo wakabaki sita.

Washitakiwa walioachwa huru baada ya kusota rumande kwa miaka minne ni Ahmed Kitabu (30), Zacharia Msese (33), Masunga Makenza (40) na Msungwa.

Inadaiwa kuwa washitakiwa hao Novemba 3, 2013, wakiwa   Msakuzi Kiswegere, Kinondoni, kwa pamoja walimuua Dk Mvungi.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo