Watu 30 kutoa ushahidi mauaji ya Dk Mvungi



Grace Gurisha

Marehemu Sengodo Mvungi
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam inatarajia kusikiliza mashahidi 30 na kupitia vielelezo 13 ikiwemo bastola moja katika kesi ya mauaji ya aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dk. Sengondo Mvungi, baada ya watuhumiwa wa kesi hiyo kusomewa maelezo ya mashahidi.

Washtakiwa hao ni John Mayunga (56), Juma Kangungu (29), Longishu  Losingo (29), Paulo Mdonondo (30) , Mianda Mlewa (40) na Msungwa Matonya (30) wote wakazi wa Dar es Salaam.

Washtakiwa hao walisomewa maelezo yao jana na Wakili wa Serikali, Patrick Mwita mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, ambapo katika maelezo hayo ya mashahidi washtakiwa hao walikiri kutenda kosa hilo.

Mwita alidai kuwa katika kesi hiyo kutakuwa na mashahidi 30 na vielelezo 13 ikiwemo bastola, mapanga matano na hati ya ukamataji.

Baada ya washtakiwa hao kumaliza kusomewa maelezo hayo, Hakimu Simba alisema washtakiwa hao watakaa mahabusu hadi tarehe ya kusikilizwa kwa kesi hiyo itakapopangwa na Mahakama Kuu katika vikao vyake.

Awali, washtakiwa katika kesi hiyo walikuwa 11 mmoja akafariki wakabaki 10, ambapo kati hao Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP), Biswalo Mganga liwasilisha mahakamani  nia ya kutokuendelea kuwashtaki washtakiwa wanne kwa hiyo wakabaki sita.

Washitakiwa hao walioachiwa huru baada ya kusota rumande miaka minne ni Ahmed Kitabu (30), Zacharia Msese (33), Masunga Makenza (40) na Msungwa.

Inadaiwa kuwa washtakiwa hao Novemba 3, mwaka 2013, wakiwa eneo la Msakuzi Kiswegere  lililopo eneo la Wilaya ya Kinondoni, washtakiwa hao kwa pamoja walimuua Dk Mvungi.

Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo