Zimamoto lakabiliwa na upungufu vitendea kazi


Celina Mathew

JESHI la Zimamoto na Uokoaji nchini limekiri kugubikwa na changamoto nyingi ikiwemo uhaba wa magari.

Jeshi hilo sasa lina magari yasiyozidi 100 wakati mahitaji yake halisi ikiwa ni magari 300, jambo ambalo linafanya kazi iwe ngumu.

Changamoto nyingine inayolikabili jeshi hilo ni uhaba wa watumishi, uelewa mdogo wa wananchi kuhusu nini kifanyike wakati linapotokea janga la moto, miundombinu mibovu ya barabara.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Kamishna Jenereli wa jeshi hilo, Thobias Andengeye alisema licha ya jeshi hilo kupata mafanikio makubwa, changamoto hizo zimekuwa kikwazo.

Alisema kwa kiasi kikubwa changamoto ya miundombinu inasababisha magari yanayoenda kuzima moto kunapotokea tatizo kuchelewa kufika sehemu husika.

Aliwataka wananchi kuwa na tabia ya kupisha magari hayo pindi yanapokuwa yakipita kwenda eneo fulani kwa lengo la kudhibiti moto badala ya kuwaambia wanaoendesha kama wana haraka wapiti juu.

Hata hivyo, alisema kwa sasa jeshi hilo lina ofisi katika mikoa 28 nchini kwenye wilaya tisa na kwamba katika miiko iliyobaki mchakato unaendelea, huku katika viwanja vya ndege vikiwa 19.

Aidha waliwataka wananchi wanaojenga nyumba kuhakikisha ramani za eneo zinapimwa ili kuwepo tahadhari ya majengo pindi moto unapotokea.

Hiyo itasidia kujua moto ukitokea wawatokea wapi ili kupunguza madhara kwa kuweka milango ya tahadhari na hadi sasa takwimu za mwaka 2016/2017 zikionesha kuwa maeneo 25,418 yameshakaguliwa,”alisema.

Aliongeza kuwa hadi sasa watu 100,000 wamepewa elimu kuhusu masuala hayo kwa shirikiana na vituo vya redio na makampuni ya simu kama Tigo, Vodacom, Airtel, Zantel na Halotel ambapo wanawajulisha wananchi kupiga namba 114 bure linapotokea tatizo.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo