Matapeli waanza kuharibu taswira ya Tanzanite


Wankyo Gati, Arusha

BAADHI ya wauzaji wa madini ya Tanzanite mkoani Arusha, wamelalamikia uwepo wa madini bandia ya Tanzanite hali ambayo imekuwa ikikwamisha soko la madini hayo.

Akizungumza na gazeti hili mmoja wa wahanga wa utapeli huo Gidion Lekasho alisema kuwa yeye alinunua madini bandia ya Tanzanite ya Sh. milioni 8.

Alisema kutokana na matukio hayo kuendelea kila siku sasa ni wakati muafaka kwa wizara ya madini kulifuatilia suala hilo hasa katika maonyesho ya madini ya vito yanayotarajiwa kufanyika hivi karibuni.

“Katika kipindi cha hivi karibuni kumekuwepo na tatizo la uwepo wa madini bandia ya Tanzanite hali mbayo inatajwa kutishia soko la madini hayo, huku baadhi ya wauzaji wakipata hasara,” alisema.

Mjiolojia  kutoka  Wizara ya Nishati na Madini Kanda ya Kaskazini, Salome Timanywa alisema madini yanapochimbwa yana umbo lake, hivyo wao kama wataalamu wanatambua kutokana na umbo la madini hayo.

Alisema wamejipanga vizuri ili waweze kukabiliana na hiyo changamoto na kuwataka wauzaji kufika wizarani ili kuweza kubaini madini feki na ambayo siyo feki.

Kaimu Kamishna wa Madini Kanda ya Kaskazini, Adam Jumaa alikiri kuwepo kwa tatizo hilo la madini bandia na kueleza kuwa katika maonyesho ya madini ya vito yatakayofanyika, tayari wana wataalamu wa kuyatambua madini hayo.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo