TRA yaja na mikakati 5 ukusanyaji kodi


Leonce Zimbandu

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imeweka mikakati mitano ya kuboresha ukusanyaji kodi ya majengo, ikiwamo kutathmini majengo ili kupanga viwango rafiki vya kodi kwa walipakodi.

Mikakati mingine ni kuimarisha usimamizi na ufuatiliaji wa ukusanyaji, kutoa elimu kwa jamii kuhusu ulipaji kodi, kushughulikia pingamizi za kodi kwa wakati na kuboresha orodha ya uthamini ili kuwa na takwimu sahihi.

Ofisa Msaidizi wa Huduma ya Mlipakodi ya TRA, Maya Magimba alisema hayo alipozungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana kuhusu umuhimu wa kodi.

Alisema kodi ni muhimu kwa Serikali kwa vile inatumika kuendesha shughuli za kijamii, ukiwamo ujenzi wa miundombinu ya barabara, zahanati na madarasa.

“Tutahakikisha nyaraka za usajili zinatunzwa na mlipakodi  kwa  kufuata taratibu ili kuepuka usumbufu,” alisema.

Alisema kodi ya majengo hulipwa kuanzia Januari mosi hadi Machi 31 kila mwaka bila adhabu, na baada ya Aprili mosi hulipwa na adhabu, kodi ya pango la ardhi hulipwa kuanzia Julai mosi hadi Desemba 31 kila mwaka.

Mkuu wa Kitengo  cha Habari na Mawasiliano Serikalini wa  Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo na Makazi, Mboza  Maige alisema  mwananchi au taasisi yenye nyaraka za umiliki wa ardhi ya Serikali anapaswa kulipa kodi hiyo.

Alisema iwapo eneo litakuwa na maendelezo ya jengo la kudumu na linatumika, mtu huyo atalazimika kulipa kodi mbili.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo