Mvua zaua watatu Dar


Celina Mathew

MVUA zinazoendelea kunyesha zimesababisha vifo vya watu watatu baada ya kuangukukiwa na kifusi kwenye machimbo ya mchanga ya Golani, yaliyopo Kigogo Fresh eneo la Pugu jijini Dar es Salaam.

Marehemu hao wa umri kati ya miaka 27-30, wawili wametajwa kwa jina moja la Amos na Shabani na mwingine Boniface Pius, ambaye mwili wake bado ulikuwa ndani ya kifusi hicho hadi jana mchana, huku Rashid Fadhili akijeruhiwa kwa kuvunjika mguu.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni alisema ilitokea juzi tisa alasiri, ambapo mmoja alijeruhiwa kwa kuvunjika mguu na kwa sasa anaendelea na matibabu.

Alisema marehemu hao wanatoka familia tofauti na mpaka jana  walishatambuliwa na ndugu zao wakati uokoaji katika eneo hilo ukiendelea ili kubaini kama kuna wengine.

“Taarifa ya kuwa kuna watu wamekufa kutokana na  kufukiwa na kifusi ni za kweli wameshaopolewa na ndugu zao wameshawatambua kwa ajili ya taratibu nyingine,”alisema.

Alisema mwili wa Pius umeshindwa kuokolewa kutokana na udongo huo kuendelea kumong’onyoka na hivyo kuleta changamoto kwenye uoakoaji, hali iliyowafanya kutafuta mbinu ya ziada kwa kupeleka Excavator, ili kujenga njia itakayokuwa na kitu kizito kitakachozuia udongo kuendelea kushuka.

Mkuu wa Wilaya hiyo, Sophia Mjema alisema machimbo hayo yalifungwa miaka miwili iliyopita lakini waliokuwa wakichimba walifanya kazi hiyo kinyemela.

Alisema shughuli hiyo ilikuwa ikiendelea katika eneo hilo kinyume cha utaratibu kwa kuwa lilifungwa hivyo wahusika walioruhusu watachukuliwa hatua za kisheria.

“Uchunguzi unafanyika kubaini viongozi walioruhusu watu kuchimba eneo hilo wakati hairuhusiwi kwa kuwa mchakato ulizuiwa siku nyingi na watachukuliwa hatua za kisheria kwakuwa hatua hiyo imeleta madhara,”alisema.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo