22% Dar watumia simu kufanya miamala


Suleiman Msuya

BENKI nyingi nchini ziko hatarini kushindwa kujiendesha kutokana na soko lake kutekwa na kampuni za simu za mkononi.

Hayo yamo katika ripoti ya hali ya uchumi nchini iliyotolewa na Benki ya Dunia (WB) juzi Dar es Salaam, ikionesha kwamba asilimia 22 ya watumiaji wa simu wanahifadhi na kusambaza fedha kupitia vifaa hivyo.

Ripoti hiyo ambayo imeanisha mambo mbalimbali kuhusu hali ya uchumi nchini imebanisha kuwa kwa sasa benki zinahifadhi asilimia nane ya fedha nchini.

Ilibanisha kuwa baada ya simu mfumo unafuata kwa kutunza fedha ni majumbani kwa asilimia 21 hasa vijijini na benki ikiwa asilimia nane.

Aidha, ripoti hiyo ya tisa kuhusu hali ya uchumi inabainisha kuwa utaratibu mwingine ambao unatumiwa kuhifadhi fedha ni kupitia familia, marafiki ambao ni asilimia mbili, Saccos asilimia moja na MFI asilimia moja.

Ripoti hiyo ilibainisha kuwa benki na taasisi zingine za fedha katika miaka ya nyuma, zilikuwa na watumiaji asilimia 11.9 ili kwa sasa wamefikia chini ya asilimia tisa hiyo ikionesha ishara kubwa ya mtu mmoja mmoja kuhamia kwenye huduma za kifedha za simu.
  
Hali kadhalika mfumo wa kupokea au kuweka fedha kupitia simu unaruhusu mteja kuweka hadi Sh milioni tatu ambapo makato hayazidi asilimia mbili hadi tano tofauti na benki ambapo inafikia asilimia 22.

Akizungumzia eneo hilo mmoja wa waandaaji wa ripoti hiyo kutoka WB, Andrea Dall’Olio alisema mabadiliko hayo ya matumizi ya simu kama njia ya kupokea na kutuma fedha, yanakuja kwa kasi kubwa duniani kote hivyo kuhitajika mifumo sahihi ya kuratibu.

Dall’Olio alisema tangu mwaka 2013 hadi mwaka juzi ongezeko la matumizi ya mitandao ya simu katika rika zote yamekuwa yakiongezeka, hali ambayo inaenda kwa kasi kubwa.

“Uhifadhi fedha katika rika zote ni asilimia 44 kwa asilimia 61, na watumiaji walio hai kwa sasa ni asilimia 91 kwa 92 na watumiaji wa huduma hizo ni asilimia 15 kwa 34,” alisema.

Aidha, akizungumzia hali ya ukopaji, alisema ripoti imebaini kuwa asilimia 63 ya mikopo inapitia marafiki, familia na majirani, kupitia simu ni asilimia 17, biashara za bidhaa asilimia 10, benki asilimia saba na zingine nyingi.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo