Kesi ya ‘Pedeshee Ndama Mtoto’ wa Ng’ombe’ yaahirishwa


Grace Gurisha

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam imelazimika kuahirisha kesi ya mfanyabiashara maarufu jijini Dar es Salaam ‘Pedeshee ndama mtoto wa Ng’ombe, Hussein Ndama (44), kwa sababu Wakili wa Serikali anayeendesha kesi hiyo hakuwepo mahakamani.

Kesi hiyo iliahirishwa hadi Aprili 27, mwaka huu, baada ya Wakili wa Serikali Mwandamizi, Shedrack Kimaro kumueleza Hakimu Mkazi Victoria Nongwa wa mahakama hiyo kuwa wakili aliyetakiwa kujibu hoja zilizowasilishwa na upande wa utetezi anaumwa, kwa hiyo aliomba kesi iahirishwe.

Upande wa Jamhuri waliwasilisha hoja kuwa hati ya mashtaka ya mfanyabiashara huyo ina upungufu wa masuala ya kisheria, kwa hiyo mahakama iitupilie mbali hati hiyo na mshtakiwa aachiwe.

Ndama anakabiliwa na makosa sita likiwemo la kutakatisha fedha haramu na kujipatia dola za Marekani 540,390 sawa na zaidi ya Sh. bilioni moja kwa njia ya udanganyifu na jana alipandishwa kizimbani akiwa amefungwa pingu, jambo ambalo liliwashangaza ndugu, jamaa na marafiki.

Ndama ambaye anatetetewa na Wakili Hashimu Rungwe anashtakiwa kuwa Februari 20, 2014 akiwa Dar es Salaam kwa nia ya kudanganya alighushi hati ya uongo ya kuuza madini nje na sampuli ya madini kwa kuonesha Kampuni ya Muru Platnum Tanzania Investment Ltd imemruhusu kusafirisha maboksi manne ya dhahabu yenye uzito kilogramu 207 yenye thamani ya dola za Marekani 8,280,000.00 zaidi ya Sh. bilioni 16 huku akijua si kweli.

Katika kosa la pili, mshtakiwa huyo anatuhumiwa kuwa Machi 6, 2014  akiwa Dar es Salaam alighushi hati ya uongo inayotoka ofisi za Umoja wa Mataifa zilizopo Dar es Salaam ya Machi 16, 2014 kwa kuonesha kuwa kilo 207 za dhahabu kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambazo zinatarajiwa kusafirishwa na Kampuni Muru kwenda Kampuni ya Trade TJL DTYL Ltd iliyopo Australia na kwamba zimesafirishwa bila jinai yoyote.

Ilidaiwa kuwa Februari 20, 2014 alighushi  nyaraka  ya malipo ya yenye namba R. 28092 ya Februari 20,2014 kwa kuonesha Kampuni ya Muru imelipa kodi ya dola za Marekani 331,200 Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa ajili ya uingizwaji wa kilo 207 za dhahabu zenye thamani ya dola za Marekanin 8,280,000 zilizokuwa zinatoka Congo huku akijua si kweli.

Ndama anatuhumiwa kuwa Februari 20, 2014 alighushi bima kutoka Kampuni Phoenix of Tanzania Assurance Ltd ya tarehe hiyo kuonesha Kampuni Muru imewekea bima maboksi manne ya dhahabu huku akijua si kweli.

Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo